Base (Swahili) |
English |
“CHAVITA itahakikisha kuwa jamii ya viziwi ina maisha bora, inayojijengea uwezo wa kujiamini, kujithamini, kujiendeleza, kukuza lugha ya alama ya Tanzania na kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za kimaendeleo, kiuchumi na kijamii kwa kushirikiana na serikali na taasisi nyingine.”
CHAVITA itahakikisha kuwa jamii ya watanzania inawatambua, inawakubali, inawathamini, inawashirikisha viziwi na kuhakikisha hawasumbuliwi na umasikini, unyanyasaji, ubaguzi na ukandamizaji wa aina yoyote”
- MALENGO YA CHAVITA
Kama wanajamii, viziwi wanayo haki ya kuchangamana na watu wengine na kushirikishwa kikamilifu katika shughuli za jamii. Hii ni haki ya msingi ya binadamu. CHAVITA itahakikisha hili kwa:
- Kuhamasisha matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi popote walipo hapa Tanzania, jamii ya watanzania, taasisi na serikali kuhusu haki za Viziwi.
- Kupigania usawa katika fursa za elimu, huduma za jamii na nyanja zote za maisha ya binadamu.
- Kupigania kutambulika kisheria kwa Lugha ya Alama ya Tanzania.
- Kujenga mwamko na kukuza matumizi ya Lugha ya Alama kwa matawi ya CHAVITA, jamii ya Viziwi nchini, na kwa jamii ya watanzania kwa ujumla.
- Kuhakikisha shughuli za maendeleo ya jamii na ki-uchumi kwa matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi nchini zinaboreshwa.
- Kuhakikisha matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi nchini wanapata uwakilishi katika ngazi zote za uongozi.
- Kufanya na kuendeleza utafiti kuhusu masuala yanayowahusu Viziwi
- Kupambana na Virusi vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI pamoja na majanga mengine yanayowakabili Viziwi.
|
- (A) Conducting all activities relating to the deaf, providing services and developing various strategies for the benefit of deaf members
- (B) The integration and educating the deaf to have a better quality of life, essential services as other citizens of the Country
- (C) To fight for justice and equality, cooperation with other organizations, government agencies and
- organizations with a goal according to our party.
- (D) collaborate with other branches directly or through the Tanzania Association of the Deaf.
- (E) To achieve the goals of CHAVITA.
- (F) To protect and respect the Constitution of CHAVITA.
- (G) To ensure the correct use of language overrides phones and used appropriately for the Deaf and interpreters in all branches. So branches yatabuni various techniques to improve and promote the use of verbal communication. Also cooperating with CHAVITA Headquarters to develop strategies to get the best interpreters capable of uniting the Deaf and other people heard.
- (H) To collect accurate data on the existing Deaf branches (mi koa / District) for their collaboration with the office of local government officials.
|