Kikao cha viongozi wa Asasi kwa ajili ya kuwaandaa washiriki kimefanyika tarehe 12/2/2011. Katika picha ni viongozi wa Kata ya Malatu na Mchemo. Viongozi hao walikuwa wanasikiliza maelekezo ya sifa za kuteua washiriki.
Katika picha Makamu Mwenyekiti Ndugu Mohamedi R Ngozi aliyesimama katika picha alifungua kikao cha viongozi wa serikali na kuwasisitiza umakini na uaminifu katika kuwaleta washiriki.
Katika picha kulia ni Mkurugenzi
Ng'onye John naye alitoa msisitizo
kuwateua washiriki kwa kuzingatia idadi.
Mtunza hazina mama Veronika Maluchila aliyesimama katika picha
aliwashukuru viongozi wote kwa mahudhurio mazuri na alisisitiza idadi waliyopewa maafisa watendaji kutoka kata za Malatu na Mchemo kuzingatia ili kwenda sambamba na bajeti ya Mradi.