Envaya

SCHOLARS FOCUS AGAINST SOCIAL  MISERIES (SFASM).

 RIPOTI MAALUM KUHUSU KIKAO CHA MRENGO (MTWARA REGION NGOs` NETWORK.)

MADA; TATHMINI YA KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA NA KIDATO CHA NNE MKOANI MTWARA.

 Hivi karibuni MRENGO waliandaa mdahalo maalum uliohusisha wadau mbalimbali wa Elimu mkoani Mtwara mnamo tarehe 08/10/2011,kuanzia saa mbili asubuhi katika ukumbi wa chuo cha ufundi maarufu kama `Masandube` ambao ulichukua takribani masaa saba, ,pia viongozi mbalimbali walialikwa ikiwemo Wabumge,Madiwani,Walimu,Wazazi na taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali.

Mjadala;

Hapo awali Mwenyekti wa MRENGO alimkaribisha mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkurugenzi wa manispaa mkoa,kisha afisa Elimu Mkoa aliwasilisha mada,hali ya maendeleo ya elimu Mkoani Mtwara,kisha azaki mbalimbali zilipewa fursa ya kuwasilisha mkakati mbadala wa kuimarisha ubora wa elimu mkoani Mtwara ikafuatiwa na majadiliano ya wadau wote juu ya nini tatizo na nini kifanyike ili kuiokoa hali ya elimu Mtwara.

Hata hivyo imeelezwa kuwa kiwango cha ufaulu hususan katika shule za msingi Mtwara kinazidi kushuka mwaka hadi mwaka kama kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa na Afsa Elimu Mkoa

Pichani (kushoto)ni mgeni rasmi Mkurugenzi wa Manispaa Mkoa akitoa hotuba juu ya maendeleo ya Elimu mkoani Mtwara, (kulia) Afsa Elimu wa mkoa wa Mtwara akitoa takwimu juu ya Elimu.

 Matatizo yaliojitokeza;

Miongoni mwa matatizo yaliojitokeza ni;

  • ·       Utoro uliokithiri 

  • ·        Mimba (kwa wasichana)
  • ·        Upungufu wa Walimu
  • ·        Upungufu wa vifaa vya ufundishaji mfano Madarasa
  • ·        Mtihani wa kidato cha pili kutokuwa na athari kwa wanafunzi

 Changamoto zingine zikiwemo,Umaskini,Mfumo mbovu wa sheria,Upungufu wa miundombinu,Uhusiana mbovu kati ya walimu na wanafunzi,Ukimwi,Mshahara(kipato) mdogo kwa waalimu na Ajira kwa watoto.

            

  Pichani ni Wanaharakati kutoka SFASM Bi Mdee Mwanaiza (kushoto) Bw.Living Anthony (Katikati).Bw Mahenge Godian (Kulia) wakichangia mada juu ya Elimu.

 Majumuisho ya mwisho ya watoa mada;

Wajumbe waliombwa kutengeneza vikundi maalumu kwa ajili ya kufanya hitimisho la nini kifanyike,kisha viongozi wa vikundi hivyo walipewa fursa maalumu ya kuwasilisha kwa maelezo.

 ·        Kuangaliwa tena kwa Sera na Sheria ya elimu nchini kwa ushirikishaji wa wadau mbalimbali wakiwemo wataalam

  • ·        Kuimarisha ulinzi na Usalama hususani katika shule za bweni
  • ·        Kuongeza kipato cha Waalimu
  • ·        Kuboresha vifaa/dhana za ufundishaji
  • ·        Kuboresha elimu juu ya mahusiano ya kimapenzi
  • ·        Kuboresha mtaala wa elimu

Kuachana na Tamaduni na Mira potofu hususani zinazomkanadamiza mototo wa kike .

Pichani(kushoto) Wadau alipewa nafasi kuunda vikundi ili kujadili nini kifanyike kukabiliana na changamoto katika Elimu (Kulia) Wadau wa Elimu kutoka Asasi mbalimbali.

 Hitimisho;  

Mdahalo ulionesha kufanikiwa kwa kiasi fulani japo viongozi mbalimbali wa kiserikali walionekana kutoitikia mualiko huo mfano Wabunge na kwa mujibu wa mwenyekiti wa MRENGO kuwa hiyo ni hali inayojirudia mara kwa mara kwa viongozi wetu.Mijadala imekuwa ikitumika kufikisha ujumbe kwa jamii au wadau mbalimbali kama walivyofanya MRENGO,lakini bado kuna changamoto ya kutotimiza mikakati hiyo kwa vitendo.

 

SFASM STUDENTS' STAND UP CAMPAIGN.

 

STUDENTS' STAND UP CAMPAIGN.

Students` Stand up campaign ni mpango wa kutoa elimu na kuhamasisha vijana hususan wanafunzi juu ya kukataa na kukemea vitendo vya rushwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi,Mpango huu ulianza rasmi katika shule ya Mayanga Sekondari mnamo tarehe 27/05/2011 chini ya SFASM kwa matarajio ya kuzifikia shule mbalimbali hasa maeneo ya Mtwara vijijini.Malengo makuu ya kuanzisha mpango huu ni kutaka kuwandaa na kuhamasisha vijana hasa Wanafunzi dhidi ya Rushwa na Maambukizi ya virusi vya Ukimwi na kuwafanya kuwa mabalozi bora katika jamii walizotoka kuanzia ngazi ya familia mpaka ya kitaifa.Vilevile mpango huu umeambatana na malengo mengine ikiwemo kuhamasisha wanafunzi juu ya elimu kwa mfano kuzingatia masomo,namna ya kujifunza na kuongeza kiwango cha kufaulu kama tatizo kubwa kwa shule za nyanda za kusini.

3.0 TATHMINI.

3.1.wanafunzi.

Wanafunzi wa Mayanga walioudhuria semina hiyo iliyotolewa na waelimishaji kutoka SFASM juu ya “Student’s Stand Up Campaign” iliyolenga kuhamasisha ukemeaji wa vitendo vya Rushwa katika mazingira ya shuleni na jamii kwa ujumla.Wafunzi wa Mayanga walionesha msisimuko mkubwa wa hamasa kwamba elimu ya rushwa kupitia semina hii waliomba iwe endelevu kwa kushirikisha taasisi mbalimbali mfano SFASM pindi mada ya rushwa inapofundishwa shuleni

                                           

Picha(a), ni Wanafunzi wa Mayanga sekondari akichangia mawazo juu ya uelewa kuhusu mada ya rushwa na picha (b) Wanafunzi waliojibu vizuri wakipokea zawadi na SFASM

      Picha(C), ni Mwenyekiti wa SFASM Bw. Anthony Living (mwenye miwani) akiwatambulisha rasmi mabalozi (Wahabi Makacha kidato cha pili na Asma Kaluma kidato cha nne) watakaowakilisha SFASM kama kikundi cha wakemea rushwa shuleni hapo, Kutokana na kuhamasika na elimu juu ya rushwa Wanafunzi waliweza kubainisha mifano mbalimbali ya rushwa inayotendeka katika mazingira yao ya shuleni na kuahidi kukabiliana nayo

 3.2.Waalimu.

Waalimu wa wanafunzi hao pia walionesha ushirikiano wa karibu na waelimishaji (SFASM) katika kufanikisha mpango kazi ulioandaliwa kwa wanafunzi hao juu ya rushwa.Mbali na waalimu hao kukubali kuwa walezi wa kikundi hicho cha wapinga rushwa hapo shuleni, pia walipendekeza SFASM kuendelea na jitihada hizo za uhamasishaji katika shule mbalimbali hususan zilizopo maeneo ya vijijini.Hata hivyo Waalimu wa shule hiyo walipewa fursa ya kutoa hamasa na wito kwa wanafunzi wao juu ya rushwa na jinsi ya kuiepuka.

 3.4 SFASM.                                       

Tathmini ya kikundi cha Wanazuoni hawa          imegawanyika katika makundi mawili ikiwemo,(a) Tathmini juu ya utayari wa Wanafunzi na Waalimu katika mada ya rushwa (b) tathmini juu ya shule na mazingira ya ufundishaji.

Katika tathmini ya utayari juu ya mada,ilionekana bayana kuwa asilimia kubwa ya Wanafunzi walionekana kuhamasika na kuelewa vizuri mada kwa uthibitisho wa kujibu maswali mbalimbali kwa usahihi yalioulizwa na Waelimishaji.Maswali hayo yaliambatana na zawadi mbalimbali ikiwemo Madaftari,Peni,Rula na Majarida yenye ujumbe juu ya rushwa.

 

Picha (d), Wanafunzi wa shule ya Mayanga sekondari (Darasani) wakifuatilia mada ya rushwa kwa makini..

 

Tathmini katika Shule ya Mayanga inaonesha bayana kuwa mazingira ya ufundishaji hayatoi morali au hamasa kwa wanafunzi hao kuelewa masomo mbalimbali kwa kiwango kinachotarajiwa,kwa mfano somo la Uraia (Civics) ambalo kuna mada juu ya rushwa kwa kidato cha pili (kwa mujibu wa mtaala wa shule za sekondari Tanzania).Hivyo ukosekanaji wa vifaa vya ufundishaji ikiwemo Vitabu,Majarida vipeperushi na ufundishwaji wa vitendo inapelekea uwelewa mdogo kuhusu rushwa.

 4, Changamoto.

Mbali na jitihada mbalimbali zinazofanywa na SFASM katika uhamasishaji juu ya kukemea vitendo vya rushwa ikiwemo kwa kutumia vyombo vya habari(mfano kumuhamasisha kijana kukataa rushwa katika uchaguzi;mwaka 2010),kuandaa semina(mfano mashuleni), kushiriki katika mada mbalimbali (mfano siku ya Wanawake duniani, Machi 8/2011) mada kuu ikiwemo “Rushwa kikwazo kikubwa katika elimu kwa maendeleo ya

mwanamke”,changamoto mbalimbali zinazojitokeza zimekuwa zikirudisha malengo ya SFASM.Miongoni mwa changamoto ambazo SFASM imekuwa ikikabiliana nazo ni ukosefu wa fedha za kufanikisha malengo tuliojiwekea,dhana na vitendea kazi kama vile Kompyuta (Computer) ,Mafaili Chombo cha usafiri,Printa(Printer) na mashine ya kutolea nakala (Photocopy machine),

Ushirikiano na mwitikio mdogo kati ya Asasi za kiserikali na za kibinafsi kwa mfano,juu ya kuviwezesha vikundi mbalimbali hususan vinavyohusu kukemea vitendo vya rushwa na vilevile mtazamo usio sahihi wa wakazi kuhusu rushwa,ikichukuliwa kama tatizo lisiloweza kuachanishwa au kupunguzwa katika jamii.

 

Picha(d), Wahamasishaji wa SFASM wakasubiri chombo cha usafiri (Pikipiki) kituo cha Iyali (Mtwara vijijini) kuelekea shule ya Mayanga umbali wa kilometa tano toka hapo kituoni

5. Mafanikio.

SFASM Imeweza kupata mihaliko mbalimbali ili kushiriki kutoa mada ikiwemo ndani na nje ya chuo cha Mt.Augustino tawi la Mtwara,pia kwa kutumia vyombo vya habari na mijadala imeweza kutoa hamasa kubwa kwa vijana kuwa na mwitikio wa uhanaharakati ili kuimarisha nguvu kazi ya Taifa.Hata hivyo imeweza kupata uwelewa mkubwa kutoka katika dawati la uelimishaji ofisi ya TAKUKURU,

 6. Hitimisho..

Mbali na changamoto mbalimbali ambazo kikundi hiki(SFASM) kinazipata,kimejiwekea malengo ya kuikomboa jamii hususani kielimu kutokana na matatizo mbalimbali kama ilivyoelezwa hapo awali kwa tathmini ya kila miaka mitano tangu ilipoanzishwa rasmi.