Habari wapendwa ktk Envaya! mzizi cultural troup tumefungua kituo cha habari na sanaa kwa vijana katika kata ya mwangata kalenga road! lengo kubwa ni kusogeza jirani na vijana huduma na taarifa juu ya afya ya uzazi na haki kwa vijana, mategemeo yetu ni kuwa na vipindi maalum kila wiki kwa makundi maalum kujadiliana juu ya afya ya uzazi na haki! tunategemea pia kuwa na siku maalum kwa wiki ambayo vijana wadogo watashindana kuandika INSHA juu ya afya ya uzazi na haki kwa vijana na mshindi atazawadiwa! Ndugu zetu ktk envaya eleweni kuwa mzizi haina mfadhili yeyote ktk kutenda haya!
Maoni (1)