Envaya

UFISADI TANZANIA

BY SIMION SIMBUJILE (MTWARA KUTOKA SHIRIKA COMMUNITY BASIC EDUCATION FOR DEVELOPMENT (COBED))
31 Mei, 2011 14:05 EAT
Kwa nini Mafisadi hawachukuliwi hatua za haraka ili watanzania wawe na imani na serikali yao sio kama sasa inavyoonekana kama wanafugwa wakati wameihujumu nchi?
BY SIMION SIMBUJILE (MTWARA KUTOKA SHIRIKA COMMUNITY BASIC EDUCATION FOR DEVELOPMENT (COBED))
31 Mei, 2011 14:06 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

@BY SIMION SIMBUJILE (MTWARA KUTOKA SHIRIKA COMMUNITY BASIC EDUCATION FOR DEVELOPMENT (COBED)): 

PHAERA (ILALA)
8 Juni, 2011 11:58 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

kwa sababu wanaopaswa kuwawajibisha ni mafisadi wenzao.

TUSPO (PUGU ILALA, DAR ES SALAAM)
8 Juni, 2011 12:01 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

Ni kweli kwa sababu mgojwa hawezi kumtibu mgonjwa mwenzake.

Sango Kipozi (Dar es salaam)
8 Juni, 2011 12:02 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

@BY SIMION SIMBUJILE (MTWARA KUTOKA SHIRIKA COMMUNITY BASIC EDUCATION FOR DEVELOPMENT (COBED)): Nakubaliana kabisa na wewe ndugu yangu. Maana mpaka sasa suala la  ufisadi limekuwa ni kama hekeya na simulizi, kwa ajili ya kuburudisha uma. Halijachukuliwa kama tatizo linalohitaji kushughulikiwa. Lazima utafutwe ufumbuzi ili kurejesha imani ya raia ambayo kwa sasa imeathirika.

Noel Mwembere (Katibu wa Elders for the prevention of Aids(EPA-UKIMWI) (MASASI, MTWARA)
26 Julai, 2011 14:19 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

Kama mapambano ya rushwa, ufisadi na Ukimwi yangepewa kipaumbele kama vile taifa lilivyopambana na ujinga(miaka ya 60), vita vya kagera (mwishoni mwa miaka ya 70),ulanguzi na uhujumu uchumi(miaka ya 80) naamini kuwa taifa letu lingekuwa mbali sana hivi sasa.


Ongeza Ujumbe Mpya

Karibisha watu kushiriki