Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

ELIMU YA STASDI ZA MAISHA.

Mimba za utotoni  na utumiaji wa dawa za kulevya  nchini Tanzania limekuwa ni tatizo linalokuwa siku hadi siku.Takwimu zinaonesha kuwa watoto wenye umri kuanzia miaka 9-25,ndio wanaoathirika kwa kiwango kikubwa na tatizo hili.

Mwaka  2008 katika shule ya msingi Ilagala mkoani Kigoma binti wa miaka tisa alionekana kuwa na ujauzito ,hali ambayo ilihatarisha maisha yake na kiumbe kilichokuwa tumboni.Mwaka 2006 wanafunzi 64 wa kike walioanza shule ya sekondari katika shule ya sekondari Ilagala,ni wanafunzi  4 tu waliobahatika kuhitimu kidato cha nne.Hapo unaweza kuona namna tatizo hili lilivyo kubwa.

Asasi za kiraia na wadau wengine wa afya  wanalojukumu la kutoa elimu kwa vijana wa shule za msingi,sekondari na wale walioko mitaani kwa lengo la kuwajengea stadi za kujitambua,kujiamini,kujithamini,na kuwajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto  zinazowakabili katika makuzi yao.

Katika makuzi ya vijana,wamejikuta wakikabiliwa na shinikizo rika,hali ambayo imewaingiza baadhi yao katika matatizo.Miongoni mwa matatizo ambayo yanawakabili vijana kutokana na shinikizo rika ni pamoja na mimba  za utotoni,utumiaji wa dawa za kulevya,ushoga,uchokoraa,na utumikishwaji katika biashara ya ngono.

Somo la stadi za maisha limeonesha uwezo mkubwa wa kuwasaidia vijana wengi kukabiliana na changamoto zinazowakabili.Vijana wengi ambao walishaanza kutumia dawa za kulenvya na kujiingiza katika vitendo vya ngono katika umri mdogo,walijiondoa  baada ya kupatiwa elimu ya stadi za maisha.

Kwa wale ambao walikuwa hawajanza vitendo hivyo,baada  ya kupatiwa elimu hiyo  wamekuwa ni waelimishaji wazuri kwa wenzao,hali ambayo imesaidia kukuza uelewa wao kuhusiana na afya ya miili yao.Stadi za maisha ni mbinu au njia anazo tumia mtu katika kukabiliana na mazingira yanayomzunguka hatimaye abaki salama kimwili,kiroho na kiakili.

Kwa kawaida stadi za maisha husaidia vijana kujiamini,kujithamini,kujiheshimu,kujitambua na kuwajenga  uwezo wa kupambanua jambo baya na zuri na kufanya maamuzi sahihi pindi wanapokabiliwa na changamoto  mbalimbali.

Katika stadi za maisha tunawafundisha vijana kutatua matatizo kwa kutumia T3.Hii ina maana kuwa

T1-----------tatizo

T2-----------tatuzi

T3----------tokeo

Katika kupata tokeo la tatizo,kuna uwezekano tokeo likawa chanya au hasi.Kwa kutumia T3 kijana anaweza kutatua matatizo kimantiki zaidi,tofauti na ambaye hana elimu ya stadi hiyo,ambapo wengi wakabiliwapo na matatizo magumu hufikia hatua ya kujiua kwa kuamini kuwa matatizo kama hayo hayana utatuzi,hususani baada ya kufukuzwa nyumbani au kukataliwa na wenzi wao.

Mada zifuatazo huwasaidia vijana kujitambua vizuri sana katika makuzi  yao.

  • Ø  Madhara ya dawa za kulevya
  • Ø  Madhara ya mimba za utotoni
  • Ø  Uthubuti wa kusema hapana yenye kumaanisha
  • Ø  Kuepuka makundi rika
  • Ø  Namna ya kuchagua rafiki mwema
  • Ø  Njia za kuepuka maeneo hatarishi.
  • Ø  Mbinu za kuepuka ushawishi wa zawadi,lifti  na pesa
  • Ø  Namna ya kujitunza wakati wa balehe na kuvunja ungo

Vijana hupata habari nyingi ambazo nyingine ni potofu kwao.Kutokana na hilo ni vema wakapewa habari sahihi zinazohusu miili ya na makuzi yao.Mfano vijana wengi wa kike na wa kiume wanapata taarifa kuwa wasipofanya ngono mapema watapata matatizo wakiwa wakubwa,habari ambazo kwa hakika si sahihi na zinapotosha.

Vilevile vijana hupenda kujaribu baadhi ya mambo ili kuona matokeo ama wanayo yasikia au kuona nini kitatokeo ya kufanya jambo fulani.Kutokana na hali hiyo wazazi,walezi,asasi za kiraia,azaki,na wadau wengine wanalojukumu la kutoa elimu kwao ili kuwaepusha na majaribio ambayo mwisho wake ni matatizo kwao.

Jeanmedia  imeliona hili na itashiriki kikamilifu kuhakikisha kuwa  inawaandaa vijana bora kwa ajili ya kuwa viongozi mahiri wa kesho.Kwa kutambua ukubwa na ugumu wa tatizo hili,jeanmedia inawaomba wadau wote kuunga mkono juhudi hizi kwa kuiwezesha kwa hali na mali ili iweze kuwafikia vijana wengi wa mjini na vijijini.

Nguvu kazi ya taifa lolote duniani ni vijana,hivyo wasipoandaliwa vizuri leo,kesho watakuwa bomu ambalo litakapolipuka litaangamiza taifa lote.Waafrika wanayo methali isemayo “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo”,hivyo kama tunahitaji kuwa na kizazi bora chenye maadili,uzalendo na uwajibikaji tuanze kuwaandaa vijana sasa kisaikolojia,kimaadili,kifikra na kimtazamo.

 

ANTON MWITA KITERERI

9 Mutarama, 2012
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (6)

alfred mwahalende (mbeya umalila) bavuzeko
Vijana wengi hudanganywa kwamba eti wasi[pofanya mapenzi katika ujana waop watasindwa kuzaa, kutokufanya mapenzi kunaleta chunusi, kufanya mapenzi kunasaidia kukomaza viungo vya uzazi pia vijana wanapotoshwa kwamba wasipofanya mapenzi viungo vyao vitaziba jambo ambalo kitaalamu siyo sahihi
19 Werurwe, 2012
alfred mwahalende (mbeya umalila) bavuzeko
upo usemi kwamba vijana ni taifa la kesho sitaki kabisa kuusikia kwani unalenga kuwarudisha nyuma vijana kimaendeleo. vijana ni tauifa la leo na siyop kesho kama wanasiasa wakongwe wanavyodai kama wakina nyerer wangesubiri kesho ati kwa wasababu ni vijana taifa lisingepata uhuru tunaojivunia leo kadhalika gadaff angesubiri leo libya isingezungumzwa hata kwenye vyombo vya habari leo. serikali na wizara zake lazima iangalie kwa kina jinsi ya kuwakomboqa vijana katika masuala nyeti kama elimu na ajira baada ya elimu. hatuna budi kuwabeza vijana kwani ndiyo nguzio opekee katiak taifa lolote lenye kupenda maendeleo duniani
19 Werurwe, 2012
alfred mwahalende (mbeya umalila) bavuzeko
VIJANA KATIKA TAIFA LOLOTE LAZIMA WAFUATE MISINGI IFUATAYO;
1.JITIHADA NA MAARIFA
2. ELIMU NA AJIRA
3UZALENDO NA MAPENZI MEMA NA JAMII
4 AMANI NA UNYENYEKEVU
5 NIDHAMU NA UTULIVU
6 NDOTO YAKINIFU NA MITAZAMO THABITI
7 HAKI NA MAMLAKA JUU YA UMILIKI
8 KIPAUMBELE NA UJASILIA MALI
9 MIKAKATI KABAMBE YA KIHARAKATI YA KUPIGA VITA UMASIKINI
10 UONGOZI BORA
19 Werurwe, 2012
alfred mwahalende (mbeya umalila) bavuzeko
PIA NAANDIKA KITABU CHANGU CHA SAFARI YA MAISHA YA KIJANA NINGEPENDA KUSHIRIKINA NA VIJANA KUTOA MAONO KWA NJIA YA SM0758051641 AU mwahalendealfred@yahoo.com
19 Werurwe, 2012
alfred mwahalende (mbeya umalila) bavuzeko
Vijana wengi hudanganywa kwamba eti wasipofanya mapenzi katika ujana waowatashindwa kuzaa, wengine wanapotoshwa kwamab kutokufanya mapenzi kunaleta chunusi, kufanya mapenzi kunasaidia kukomaza viungo vya uzazi pia vijana wanapotoshwa kwamba wasipofanya mapenzi viungo vyao vitaziba jambo ambalo kitaalamu siyo sahihi. hali kadhalika vijana wanapotoshwa kwamba lazima wafanye mapenzi na wachumba wa kabla ya ndoa ili kuwajua vizuri.siyo siri vijana wamedanganyiak padogo kwani wanadanganywa na mambo madogo hebu fikilia kijana anyeyreambiwa eti usipofanya ngono uume utapunguaz na kuwa mdogo
19 Werurwe, 2012
Hafidh (Kwa vijana) bavuzeko
Katika maisha kuna ki2 kinaitwa paspective [taswira] kwa vijana walio wengi huwa hawana muono katka maisha mpaka afikwe na matatizo ndio aelewe hvy ningependa vijana wapate ilimu ya jinsia hata life skill, kwa kwel vijana kupitia ktk changamoto za baleghe huwa ni kipindi cha tabu sana lakin kini sirikali ikitowa elimu za kijami mashulen mara kwa mara basi hata matatizo yatapungua kwa kiasi kikubwa.
27 Kamena, 2012

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.