Envaya
Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

FCS Narrative Report

Utangulizi

IRINGA CIVIL SOCIETY ORGANAZATIONS -UMBRELLA
ICISO- UMBRELLA
KUIMARISHA MAHUSIANO KATI YA AZAKI, WAWAKILISHI WA WANANCHI NA WATENDAJI WA SERIKALI ILI KURESHA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI
FCS.MG/3/07/108
Tarehe: 31 Dec 2010 hadi 15 April 2011Kipindi cha Robo mwaka: ROBO YA SITA
ERIKO KAWANGA
P.O.BOX 317,
IRINGA.

Maelezo ya Mradi

Utawala Bora na Uwajibikaji
Mradi huu unakidhi kwa kuwawezesha wananchi kuondokana na woga waliokuwa nao wa kuogopa kuwahoji watendaji na viongozi wao kuhusu utendaji na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kijamii na za maendeleo pale wanapoona mambo yanakwenda kinyume na matarajio yao
MkoaWilayaKataVijijiIdadi ya Wanufaika
IringaIringa Manispaa168655
Mufindi Kaskazini71043
Mufindi Kusini61154
Ludewa5870
Kilolo101547
Isimani31071
Makete71460
Njombe Kusini51138
Njombe Kaskazini7746
Njombe Magharibi91445
Kalenga5751
 Walengwa wa moja kwa mojaWalengwa wasio wa moja kwa moja
Wanawake2061030
Wanaume3741735
Jumla5802765

Shughuli na Matokeo ya Mradi

- Wananchi watapata fursa ya kupata mrejesho wa mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiwatatiza
- Itakuwa fursa nyingine ya mwananchi kutoa maoni yao na kuuliza maswali juu ya mambo yanayowasibu
- Utakuwa ni mwanzo wa kujenga mazozea ya mikutano kama hiyo
kufanya mikutano baina ya wananchi, watendaji, wana Azaki na watunga sera (Wabunge na Madiwani)
Mikutano 11 imefanyika katika majimbo yote ya uchaguzi 11 na wananchi 580 wameshiriki kutoka Halmashauri 8, kata 78 na vijiji 107
- Kutokana na majukumu mbalimbali ya kiutendaji, baadhi ya wabunge hawakuweza kushiriki bali waliwatuma wawakilishi wao ambao walipeleka mrejesho wa yote yaliyozungumzwa kwenye mkutano . Pamoja na njjia hiyo ICISO iliweka kumbukumbu ya kila kilichoongelewa /kuulizwa na kupeleka taarifa kamili kwa Mbunge
- Pamoja na kufuatiliwa kwa kipindi kirefu ili kupanga muda muafaka wa kila Mbunge kuweza kushiriki katika mkutano, baadhi hawakushiriki wala kutuma wawakilishi lakini ICISO imewapelekea taarifa ya mwenendo mzima wa mkutano ulivyoendeshwa
Kufanya mikutano/midahalo ya kijimbo - Kiasi cha fedha kilichotumika Tsh. 16,540,000/=
Ufuatiliaji na tathmini - Kiasi cha fedha kilichotumiuka Tsh. 1,496,000/=
Gharama za Utawala Kiasi cha fedha kilichotumika Tsh. 37,290,000

Mapato na matumizi mchanganuo wake upo kwenye kiambatanisho (attachment) mwisho wa taarifa.









Mafanikio au Matunda ya Mradi

-Wananchi wamepata mwamko wa kudai haki zao (ikiwa ni pamoja na mikutano na Wabunge
- Wawakilishi wa wananchi (Wabunge, madiwani pamoja na watumishi wa Halmashauri) wameona umuhimu wa kushirikishana/kukutana ana kwa ana na wananchi katika uibuaji, kufanya maamuzi na kufuatilia utekelezaji
- Mahusiano kati ya Azaki, wawakilishi, Watendaji wa Serikali na wananchi yameboreka na kuimarika ili kulea maendeleo kwa kasi
- Wawakilishi wa wananchi pamoja na watendaji wa Serikali wameona uzuri wa kupata maoni ya wananchi kabla na baada ya kufanya maamuzi kwa njia iliyowazi na shirikishi
- Wananchi wameuliza maswali na kueleza kero zinazowakabili bila woga
- Wananchi wamedai midahalo kama hii iandaliwe mara kwa mara ili watu wengi wapate fursa ya kushiriki
- Wananchi wameeleza kuwa utaratibu uliopo sasa wa Wabunge kutembelea sehemu mbalimbali (sio nyingi) hautoi mwanya wa kuuliza maswali na kero zao maana unakuwa wa kimsafara- kufika, kusalimia na kuwashukuru kwa kuchaguliwa na kufanyiwa sherehe fupi ( na watu wa chama chake) na kuondoka kwenda vijiji vingine
- Wananchi wamesema mikutano ya kijiji huwa haiitishwi, huu umewapa fursa ta kueleza shida zao. Wanadai mikutano.
-Baadhi ya Wabunge, MAdiwani na watendaji wa Halmashauriwamesema wamesema wamefaidika kukutana na wananchi kutoka vijiji mbali mbali kwa mara moja na kupata maoni na kero zao pia wao watafikisha taarifa mbalimbali kwa wenzao kwa urahisi
- Mikutano hii imezidi kuimarisha mahusiano na mashirikiano kati ya wananchi, Azaki, wawakilishi na watumishi wa Halmashauri
- Pamoja na kuwepo mgawanyiko wa kiitikadi katika jamii hasa vijijini, mtu akiuliza swali au kuongelea kero inayogusa jamii kwa ujumla, alishangiliwa sana na umati wote uliohudhuria
- Mikutano mingine ikiitishwa huwa inaendeshwa kiitikadi zaidi maana watu wa vyama vya ushindani huonekana kama wachochezi wanapohoji mambo ya msingi na mara nyingi hunyimwa nafasi ya kuongea
- Wananchi wameimarishana na kutiana moyo katika kutetea na kudai haki zao
(Hakuna jibu)

Mambo Mliyojifunza

Maelezo


Baadhi ya viongozi wa vijiji na hata kata huwa hawaitishi mikutano kwa kuogopa kuulizwa maswali ambayo hawana majibu yake maana wanafahamu ukiukaji walioufanya


Dola inawajengea uadui wanaharakati wanaotaka kuanzisha shughuli za maendeleo maana wakifanikiwa itawajenga hivyo inawazuia wananchi kunufaika


Mradi umethibitisha kuwa wanyonge na wasiojiweza bado wanaendelea kukosa haki zao mbele ya watensaji wa Serikali mfano:-
(a) Katika mji wa Makambako (Jimbo la Njomba Kaskazini) mwanamke mjane aliulizia kujenga nyumba ya kuishi na familia yake- alizuiliwa na Mkurugenzi kwa kumwambia haparuhusiwi kujengwa chochote lakini baada ya siku chache tajiri mmoja ameruhusiwa kujenga
(b) Mjini Makambako, kuna eneo walizuiliwa wafanyabiashara kujenga na kufunga mashine za kukoboa mpunga kwa sababu ya kulinda afya za wananchi KUZUIA VUMBI) lakini baada ya siku chache tajiri mmoja aliruhusiwa kujenga ghala la kuhifadhi simenti! FEDHA/RUSHWA INAPOFUSHA NA AFYA ZA WANANCHI ZIMEINGIA HATARINI ZAIDI


Baadhi ya wachabuliwa (Wabunge na Madiwani) huwanyanyapaa kwa kuwanyima huduma watu walio katika maeneo ambayo walipata kura chache jambo ambalo ni kinyume na utawala bora




Katika maeneo ya utawala ambayo viongozi wanatoka familia moja, mwananchi akipeleka matatizo anaundiwa visa kwa kulinda maslahi ya familia yao. Wananchi hawana mahali pa kukimbilia kutatuliwa matatizo yao. (Kata ya Mdandu, Wilaya ya Wanin'gombe Diwani mwanamke na mume wake ni Katibu Kata, Shule ya Sekondari Mazombe katika Wilaya ya Kilolo, Mwanaume ni Mwenyekiti wa bodi ya shulke wakati mkewe ndiye mkuu wa shule


Wananchi wamewatuhumu baadhi ya viongozi wao kutopendelea wananchi kuhudhuria katika mikutano na kushiriki kwa kuuliza maswali. Hutuma watu wa kuangalia nani alihudhuria na kuzungumza mambo gani, akiambiwa kuwa alilalamikiwa na mtu fulani basi mtu huyo huandamwa na manyanyaso

Changamoto

ChangamotoNamna mlivyokabiliana nazo

Baadhi ya Wabunge kutokuwa tayari kushiriki katika mikutano tarehe tulizopanga na hivyo kuchelewesha utekelezaji wa Mradi

-Tuliwashirikisha Wabunge tukapanga pamoja tarehe walizoona zinaendana na mipango yao.


Pamoja na kushirikisha Wabunge kupanga siku za kufanya mikutano wengine walibadili ratiba


Tuliwakubalia mabadiliko na kupokea mapendekezo yao mapya ya kufanya mkutano


Baadhi ya Wabunge hawathamini mikutani- wanasema wanataratibu zao za kukutana na wananchi


a)Tulishirikiana na watu walio karibu na wabunge hao ili wawashawishi waweze kushiriki- tulifanikiwa kwa baadhi
b) Sehemu nyingine tuliwatumia Wenyeviti wa Halmashauri/Madiwani, Makatibu wa Wabunge na Watendaji wa Halmashauri


Baadhi ya viongozi na watendaji wa Halmashauri za Wilaya kupata jazba kutokana na maoni ya wananchi


Tuliwaelimisha kwamba hiyo ndiyo hali ya watanzania wa leo hivyo inahitaji uvumulivu


Baadhi ya Halmashauri za Wilaya kutokuwa tayari kuoa kumbi na kutoza gharama kubwa


Tulitafuta kumbi na maeneo mengine


Baadhi ya viongozi wa Mitandao ya Azaki kuonyesha wazi wazi ushabiki wa vyama vya siasa hali iliyosababisha kutokubalika wakati wa maandalizi wa shughuli za Mradi

Tuliwashauri wajirekebishe na kutumia viongozi wengine wa mitandao


Bado watendaji wa Serikali wanadai posho kubwa kwa mujibu wa vyeo vyao


Tulizidi kuwaelimisha kwamba shughuli za Azaki ni za kujitolea na pia tuliwakumbusha kwamba ni sehemu ya wajibu wao kuhudhuria mikuano inayohudhuriwa na wananchi


Mahusiano

WadauNamna mlivyoshirikiana nayo


Wakuu wa Wilaya


Kila Wilaya tulipokwenda kuendesha mikutano tuliwatembelea wakuu wa Wilaya kuwaelezea madhumuni ya mikutano tunayoifanya na hatimaye kuwaomba wawe wageni rasmi kufungua na hata kushiriki


Wakurugenzi wa Halmashauri


a)Kila mkutano tulioendesha wakurugenzi husika walialikwa kushiriki- wengi watuma wawakilishi, pia tulishirikiiana nao katika maandalizi ya awali
b)Watumishi wa idara mbali mbali walishiriki kwa kujibu maswali na hoja zilizojitokeza na kuchukua yale yaliyohitaji kufanyiwa kazi


Wenyeviti na Madiwani wa Halmashauri


Walialikwa kushiriki katika mikutano na baadhi walihudhuria na kutoa majibu na ufafanuzi kwa baadhi ya mambo yaliyojitokeza


Watendaji wa Kata na vijiji


Walishirikiana na viongozi wa mitandao kuteua washiriki

(6) Asasi


(7) Mitandao

(8) Wafanyabiashara

(9) Jamii

(10) FCS

Walishiriki kwenye midahalona kusaidia kuteua washiriki


Mitandao ya Wilaya ambayo ni zao la Asasi ndiyo ilikuwa kiungo kikuu cha mawasiliano na Waheshimiwa Wabunge kupanga siku ya Mkutano. Kuandaa kumbi za Mikutano, kuteua washiriki kwa kufuata vigezo na hatimaye kuandaa na kusambaza barua za mialiko kwa washiriki wote

Walisadia kutuwezesha kupata kumbi, viburudisho na vyombo vya mawasiliano, usafiri na vyakula

Ndio walengwa na wanufaika wa Mradi, walishiriki katika mikutano na kutoa mawazo, maoni, kuuliza maswali na kupata majibu

Wametoa ruzuku

Mipango ya Baadae

(Hakuna jibu)

Walengwa Waliofikiwa

    Walengwa wa moja kwa mojaWalengwa wasio wa moja kwa moja
Wajane na WaganeWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watu wanaoishi na VVU/UKIMWIWanawake420
Wanaume630
Jumla1050
WazeeWanawake37175
Wanaume67335
Jumla104510
Watoto YatimaWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
WatotoWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watu wenye UlemavuWanawake315
Wanaume525
Jumla840
VijanaWanawake149745
Wanaume2741370
Jumla4232115
Watu wengineWanawake1265
Wanaume22110
Jumla34175
(Hakuna jibu)

Matukio Mliyoyahudhuria

Aina ya TukioLiniMambo uliyojifunzaHatua zilizochukuliwa
Training24-25 April 2008Financial and record keeping, Record cycle, Basic of report writing,Logframe & Monotoring and EvaluationUsing the skills I learnt to prepare reports we submmit to FCS.
Tamasha la ASASI (Ubungo Plaza)27-29 Oktoba 2009Mikakati ya Utendaji ya FCS inavyolenga CSOsFCS siyo mfadhili wa CSOs bali ni Mshirika wa CSOs katika kuiletea jamii maendeleo na kuzijengea uwezo asasi.Imekuwa rahisi kwetu kushirikiana nayo katika mambo mengi.
Mafunzo12-13 Nov.2009Tathmini ya Uwezo wa AZaKiTunaitumia kujitathimini
MafunzoNjuweni HotelPETSTrained Councillors,CSOs and Council Workers on PETS skills and later they conducted practical PETS on EDUCATION and HEALTH ni their respective Councils and presented their findings to the councils commettee for education,health and water.

Viambatanisho

Ifuatayo »

Maoni (1)

Mr. Bartolomew M.Kunzugala (Iringa Municipality a Southern Highlands Zone Head Office.) alisema:
Research, Planning and Project Write- Up Association (RPPW) - NGO of Southern Highland Zone Branch with its Office in the Moshi University College of Cooperative and Business Studies (MUCCOBS) congratulates FCS on its efforts in incapacitating Civil Societies for ensuring that people of Tanzania are well trained in various aspects such as Good Governance, Policies and Laws, Government's responsibilities and accountabilities to the the citizens, as well as the citizens to vice versa.
We also comment the efforts done by Iringa Civil Society Organization -ICISO on the project which touched the residents of the formally Iringa Region which have been divided into two regions (Iringa and Njombe resp); each comprising Four Former Local District Authorities.
6 Julai, 2012

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.