Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations
  • UTUME WA CHAVITA-MISSION

  

CHAVITA itahakikisha kuwa jamii ya viziwi ina maisha bora, inayojijengea uwezo wa kujiamini, kujithamini, kujiendeleza, kukuza lugha ya alama ya Tanzania na kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za kimaendeleo, kiuchumi na kijamii kwa kushirikiana na serikali na taasisi nyingine.”

                                                      

  • DIRA YA CHAVITA-VISION

  

CHAVITA itahakikisha kuwa jamii ya watanzania inawatambua, inawakubali, inawathamini, inawashirikisha viziwi na kuhakikisha hawasumbuliwi na umasikini, unyanyasaji, ubaguzi na ukandamizaji wa aina yoyote”

 

  1. MALENGO YA CHAVITA

 

Kama wanajamii, viziwi wanayo haki ya kuchangamana na watu wengine na kushirikishwa kikamilifu katika shughuli za jamii. Hii ni haki ya msingi ya binadamu. CHAVITA itahakikisha hili kwa:

 

  • Kuhamasisha matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi popote walipo hapa Tanzania, jamii ya watanzania, taasisi na serikali kuhusu haki za Viziwi.
  • Kupigania usawa katika fursa za elimu, huduma za jamii na nyanja zote za maisha ya binadamu.
  • Kupigania kutambulika kisheria kwa Lugha ya Alama ya Tanzania.
  • Kujenga mwamko na kukuza matumizi ya Lugha ya Alama kwa matawi ya CHAVITA, jamii ya Viziwi nchini, na kwa jamii ya watanzania kwa ujumla.
  • Kuhakikisha shughuli za maendeleo ya jamii na ki-uchumi kwa matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi nchini zinaboreshwa.
  • Kuhakikisha matawi ya CHAVITA na jamii ya Viziwi nchini wanapata uwakilishi katika ngazi zote za uongozi.
  • Kufanya na kuendeleza utafiti kuhusu masuala yanayowahusu Viziwi
  • Kupambana na Virusi vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI pamoja na majanga mengine yanayowakabili Viziwi.
Latest Updates
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA updated its History page.
Ilianzishwa kama klabu ya viziwi ambayo watu walikuwa wanaidharau na kusema ni machizi (vichaa) – Baadae ikaanzishwa kikundi cha viziwi likijulikana kama kikundi cha viziwi kondoa (kiviko). – Baadae CHAVITA) mkoa Dodoma walitoa mafunzo ya lugha ya Alama (L.A.T)katika tawi la wilaya ya kondoa ndipo likaanzishwa CHAMA CHA... Read more
December 10, 2012
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA added a News update.
Chavita imetoa mafunzo ya Lugha ya Alama kwa Taasisi za serikali na Wazazi wanaoishi na Watoto Viziwi katika kata 5,ambazo ni Bereko,Kondoa mjini,Pahi,Kilimani na Chemchem katika Wilaya ya Kondoa. Mafunzo ya lugha ya alama kwa Taasisi za... Read more
December 10, 2012
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA created a Home page.
UTUME WA CHAVITA-MISSION CHAVITA itahakikisha kuwa jamii ya viziwi ina maisha bora, inayojijengea uwezo wa kujiamini, kujithamini, kujiendeleza, kukuza lugha ya alama ya Tanzania na kushiriki kikamilifu katika... Read more
December 10, 2012
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA added a News update.
Jamii yetu ifahamu matumizi ya lugha ya Alama kuwe na uwiano wa mawasiliano kati yetu (viziwi na jamii nyingine). – Kutetea haki ya viziwi kwa vyombo ya usalama,mahakama na polisi ili kuwatambua jamii ya viziwi. – Kujenga ushirikiano na taasisi (asasi) mbalimbali ili kuwawezesha kulitambua kundi hili. ... Read more
April 27, 2012
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA added chama cha viziwi tanzania to its list of Partner Organizations.
December 22, 2011
CHAMA CHA VIZIWI TANZANIA (CHAVITA) WILAYA YA KONDOA added a News update.
Kuna changamoto kubwa katika kundi letu la Viziwi kutokutambulika hata Vijijini kutokujua hasa umuhimu wa watoto Viziwi kwenda kupata elimu ya awali,msingi na sekondari na hata Ufundi.Na changamoto zingine Viziwi wanatakiwa kuwezeshwa ili wafikie malengo yao ya milenia mpyaViziwi wengi tuko nyuma kimaendeleo lisha ya kuwa... Read more
December 22, 2011
Sectors
Location
Kondoa , Dodoma, Tanzania
See nearby organizations