Log in
ASASI YA UKOMBOZI WA VIJANA TANZANIA ( AUVITA)

ASASI YA UKOMBOZI WA VIJANA TANZANIA ( AUVITA)

Bunda, Tanzania

MISITU NI UHAI

ASASI YA UKOMBOZI WA VIJANA TANZANIA ( AUVITA)
February 14, 2014 at 9:49 AM EAT (edited March 5, 2014 at 9:31 PM EAT)

HIFADHI NA MATUMIZI ENDELEVU YA MISITU

Misitu ni nini?

Misitu ni ardhi yoyote yenye uoto wa mimea na wingi wa miti ya kimo

chochote ivunwayo na isiyovunwa na iliyo na uwezo wa kutoa timbao au

mazao mengine yenye kurekebisha hali ya hewa au mfumo wa vyanzo vya

maji au yenye kuhifadhi mifugo au wanyamapori

Msitu wa hifadhi

Hili ni eneo la misitu, aidha kwa uzalishaji wa mbao na mazao mengine ya

misitu, ama ni kwa ajili ya ulinzi wa maeneo muhimu yenye lindimaji chini ya

udhibiti wa sheria ya misitu baada ya kutangazwa na waziri mhusika.

Matumizi endelevu ya misitu

Maana ya matumizi endelevu ya misitu

Matumizi endelevu ya misitu ni utumiaji wa maliasili zilizopo kwenye msitu

pamoja na kuendelea kuzizalisha maliasili hizo bila kuathiri uwepo wake.

Katika matumizi endelevu kwa kawaida kiasi kinachovunwa hakizidi uwezo

wa eneo lile wa kuzalisha maliasili hizo. Kwa maana hiyo, japokuwa maliasili

hizo zinatumiwa, ni rahisi kuwepo kwa ajili ya vizazi vijavyo ikiwa matumizi

yake ni endelevu.

Namna ya kufanya matumizi endelevu ya misitu

Kuna njia mbalimbali za kuhifadhi na kutumia misitu katika njia endelevu

kama ifuatavyo:

Ushirikishwaji wa wananchi katika kusimamia na kuhifadhi misitu

Maana ya usimamizi shirikishi wa misitu

Usimamizi Shirikishi wa Misitu (USM) unahusu utaratibu wa kusimamia

misitu ambapo jamii inahusika kwa sehemu kubwa katika

utekelezaji.Usimamizi huu unaweza kuwa kwenye misitu iliyohifadhiwa

ndani ya ardhi ya kijiji au ardhi ya jumla au kwenye misitu ya hifadhi ya

serikali

Sababu za ushirikishwaji

Lengo kubwa la usimamizi shirikishi wa misitu ni kuwashirikisha wananchi

katika kuendeleza kuhifadhi na kutumia misitu kwa vizazi vilivyopo na

vijavyo. Hapo awali wakati wa sheria za misitu za kikoloni shughuli za

kuhifadhi misitu ziliendeshwa kama za kijeshi na hivyo kujenga mawazo

kuwa misitu ni mali ya serikali na wananchi hawahusiki. Kutokana na hali

hiyo wananchi hawakuipenda misitu iliyowazunguka na walijenga uadui

mkubwa baina yao na watendaji wa idara ya misitu matokeo yake

uharibifu wa misitu uliendelea kwa kiasi kikubwa. Kwa kuwa watumiaji

wakubwa wa misitu ni wananchi wanaoizunguka, serikali iliona ni vyema

ikawashirikisha wananchi wake katika swala zima la kuhifadhi ndiyo

maana siku hizi wananchi wanashiriki kwenye suala la kuhifadhi misitu

kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kutoa maamuzi. Swala la ushirikishaji

limeainishwa kwenye sera ya taifa ya misitu (Forest policy) ya mwaka

1998 na sheria ya misitu (Forest Act ya mwaka 2002)

Faida za ushirikishwaji

Faida za ushirikishwaji wananchi kwenye kuhifadhi misitu zipo nyingi

ikiwa ni pamoja na wananchi kushiriki kwenye kufanya maamuzi

kuhusu misitu yao, Kupata fursa ya kujipatia mazao ya misitu kama

kuni, madawa, matunda na mboga bila vikwazo, wananchi kupewa

fursa ya kanzisha misitu yao ya hifadhi kama vile misitu ya hifadhi ya

kijiji, ya vikundi na hata ya mwananchi mmojammoja.

Kwa upande mwingine serikali inanufaika kwa kuwa inaongezewa

nguvu na wananchi katika kuhifadhi misitu. Idadi ya misitu katika

Tanzania ni kubwa sana ukilinganisha na idadi ya watumishi wake

hivyo kwa kuwashirikisha wananchi wanasaidia katika swala zima la

kulinda misitu ili isiharibiwe na wahalifu wenye nia mbaya.

Matumizi ya mila za jadi katika kuhifadhi misitu

Matumizi ya mila za jadi kama tambiko yamechangia kwa kiasi kikubwa

kulinda misitu katika maeneo ya Usambara na sehemu nyinginezo

mbalimbali Tanzania kwa kuwa maeneo yanayotumika kwa shughuli za jadi

yamekuwa yakipewa heshima ya pekee. Kwa mfano wanavijiji na wazee wa

tambiko wamekuwa wakipanga faini kama za mifugo au pombe na hata fedha

kwa yeyote aliyejaribu kukiuka kanuni za utunzaji wa maeneo haya muhimu.


Add New Message

Invite people to participate