Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Icyongereza. Edit translations

TANZANIA NA UZALENDO WETU TUMEKOSEA WAPI?

Uzalendo ni kitendo cha mtu kuipenda nchi yake, rasilimali zilizomo na watu wake kwa moyo wa dhati kwa kuilinda, kuithamini wakati wote na mahali popote.

Uzalendo katika nchi ndio chanzo cha maendeleo na usawa kwa watu wote nchini. Uzalendo unaleta haki, uzalendo unajenga misingi ya kujaliana, uzalendo ndio chachu ya matumizi ya rasilimali za nchi kwa usawa, uzalendo unatujengea undugu na amani, uzalendo unajenga na kudumisha upendo, uzalendo unajenga na kudumisha ushirikiano, uzalendo unajenga misingi ya uwajibikaji kwa wanajamii, uzalendo huondoa unyonyaji na matabaka katika jamii.

Uzalendo ni upendo na dhana ya hiari ya mtu binafsi uzalendo hujengwa kutoka moyoni mwa mtu, wakati mwingine uzalendo hujegwa na wanajamii kipitia misingi ya maisha wanayoyaishi na itikadi ya kisiasa  miongoni mwa wanajamii. Hivyo mtu anaweza kuzaliwa akiwa mzalendo au  itikadi ya kisiasa na misingi ya maisha katika jamii inaweza kumjenga mtu katika hali ya uzalendo.

Uzalendo unagawanywa katika aina mbili; a) uzalendo wa kihistoria ambao unatokana na maisha ya watu waliotangulia katika jamii. b) uzalendo wa kiutu. Huu ni uzalendo ambao huchukulia binadamu kama alivyo. Mfano katika Biblia maandiko yanasema mpende jirani yako kama nafsi yako.

Katika taifa letu dhana ya uzalendo imepotea miongoni mwa wanajamii. Historia inaonesha Tanzania imepitia vipindi mbalimbali; kipindi cha kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni, wakati wa kupigania uhuru na  wakati baada ya uhuru. Kila kipindi kilijengwa na misingi yake ya uzalendo.

Kipindi kabla ya ukoloni historia inaonesha kuwa mababu zetu waliishi katika misingi ya umoja mshikamano na undugu, walifanya kazi kwa kushilikiana waliishi kama wamoja, rasilimali ziliwanufaisha wote watu wote walikuwa na haki sawa katika utumiaji wa rasilimali. Kipindi hiki kilitawaliwa sana na uzalendo wa  kiutu.

Kipindi cha ukoloni. Historia inaonesha kuwa kipindi hiki wakoloni walitumia kila mbinu kuuvunja na kuundoa kabisa uzalendo miongoni mwa wanajamii. Walitujengea mioyo ya chuki, walituondolea umoja, walitujengea ubaguzi, walitugawa ili watutawale. Yote haya waliyafanya kwa manufaa yao binafsi ya kuzinyonya rasilimali za waafrika, walitumia Ardhi yetu kujinufaisha , walitumia  udhaifu wetu kutufarakanisha, walitujengea matabaka katika jamii. walichonacho walikuwa nacho na wasiokuwa nacho waliendelea kukosa, elimu ilitolewa kwa misingi ya ubaguzi katika jamii, rasilimali za nchi zilitumika kuwanufaisha wachache wenye vyeo na madaraka tu. Hakika wakoloni walifanikiwa kutufarakanisha waafrika na kutuondolea uzalendo wetu.

Wakati wa kupigania uhuru. Hiki ni kipindi ambacho  waafrika wenyewe tulianza kujijengea  mioyo ya uzalendo tulioupoteza kupitia ukoloni, tulijijenga pamoja kushirikiana na kupambana dhidi ya ukoloni. Kipindi hiki mioyo ya uzalendo ilijegwa upya katika jamii ya watanzania. Baba wa Taifa alitumia juhudi zake kupitia Chama cha TANU kutuunganisha pamoja , tuwe wamoja , kutujengea upendo na baadae kushirikiana kudai uhuru wetu tukiwa kitu kimoja na wamoja.

Waasisi wetu walitumia juhudi zao kuujenga uzalendo na upendo katika jamii wakaiacha mizizi kwa mategemeo kwamba kizazi kilichofuata kingeendeleza hali ile.

Tanzania ya sasa si ile ya waasisi wetu, uzalendo tuliojengewa hatunao tena, umoja na mshikamano vimepotea sasa kila mtu akwenda kivyake nchi inapoteza mwelekeo , umasikini unakua kiuhalisia lakini unapungua kitakwimu, matabaka yanazidi kuongezeka makuadi wa kupoteza uzalendo wetu wanaongezeka kila siku, rasilimali sasa zinawanufaisha  watu baadhi. Kwa mioyo migumu waliyo nayo sasa hata madaraka wanarithishana ili tu kujilinda.  Taifa linahitaji jitihada za kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa tunautetea na kuuendeleza uzalendo wetu kwa maendeleo yetu . matabaka tuyaonayo leo ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo miongoni mwetu, misingi ya utu, ummoja, undugu sasa tumeipoteza kila mtu anafanya ajualo. Mabadiliko yanaletwa na mimi na wewe tumia nafasi yako vizuri kujenga usawa, utu, uwajibikaji, undugu katika jamii kwa maendeleo ya Taifa letu.

 

 

 

 

7 Gashyantare, 2015
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (2)

Maisha Pa1 (Kahama-Shinyanga, Tanzania) bavuzeko
Ni kweli wana asasi ya Ukomboz wa Vijana, hata sisi vijana wa taasisi ya Maisha Pa1 tunaungana nanyi, uzalendo haupo kabisa katika nchi yetu kwa sasa, hakuna shughuli za kijamii zilizowashirikisha wazee wetu wa miaka ya nyuma kama kujadilia maendeleo ya kijiji kwa kukaa chini ya mti, kutengeneza barabara, kuchimba visima, kujenga shule N.k
8 Gashyantare, 2015
Daudi Masui (Der es salaam(mbezi,goba)) bavuzeko
Makara iyo apo juu.imebeba ujumbe mzito sana kwa anae ona na kufahamu maana asa ya UZALENDO.kiukweli katika jamii yetu uzalendo haupo kwa vijana wa Tanzania kwa kizazi iki cha sasa,na hii utokana na vijana wenyewe kutojua uzalendo ninini??ninauwakika na ninacho kisema asilimia miya moja vijana wengi wa Tanzania atujui uzalendo ninini.maana anayefahamu maana ya uzalendo,anamipaka ndani yake atajua uzalendo nkwajili ya nchi tu na siyo na vilivyomo .kwaiyo kazi ya kwanza ya kufanya nikuamasisha saana na kufundisha faida za uzalendo na umuhimu wa mtu mmoja mmoja kuwa mzalendo na jamii kwa ujumla asante.
31 Nyakanga, 2019 (edited 31 Nyakanga, 2019)

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.