Fungua
Concern for Women and Children Development Initiative

Concern for Women and Children Development Initiative

Kilimahewa, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

FCS Narrative Report

Utangulizi

Concern for Women and Children Development Initiative
WIDEK
Kuimarisha uwajibikaji na utendaji wa shughuli za asasi.
FCS/RSG/1/11/167
Tarehe: Agosti – Oktoba 20011Kipindi cha Robo mwaka: Robo ya kwanza
Kagama Hamisi
S.L.P 258, Kigoma
MOB: 0754600724/ 0715600724
Email: widektz@gmail.com

Maelezo ya Mradi

Uimarishaji Asasi za Kiraia
Mradi huu umeiwezesha asasi yetu ya WIDEK kufikia malengo yake kwa kua na uwezo katika maswala ya uandaaji na uendeshaji wa miradi (Project design and Management), Uandishi wa taarifa mbalimbali na miradi, Uendeshaji wa asasi (Organisation development, Utunzaji na uandishi wa vitabu vya pesa, na asasi kuwa na muongozo wa pesa na mpango mkakati wake.
Hivyo asasi imeweza kuongeza ufanisi katika utendaji na utekelezaji wa shughuli zake za kila siku.
MkoaWilayaKataVijijiIdadi ya Wanufaika
KigomaKigomaMwanga KusiniMtaa wa Kilimahewa26
 Walengwa wa moja kwa mojaWalengwa wasio wa moja kwa moja
Wanawake25(Hakuna jibu)
Wanaume01(Hakuna jibu)
Jumla26(Hakuna jibu)

Shughuli na Matokeo ya Mradi

1.1. Wanachama 20 na viongozi 6 Jumla yao 26 wa asasi wameelewa uandishi na
usimamiaji wa miradi na fedha, na wameanza kuandika miradi na kuituma kwa wafadhiri.

2.1. Mpango mkakati wa asasi umeandaliwa.

3.1 Viongozi 6 na wanachama 20 jumla yao 26 wa asasi wameelewa uendeshaji wa asasi,
majukumu ya viongozi na wanachama katika usimamizi wa shughuli za asasi.

3.2 Wanachama na viongozi jumla 10 wameshiriki katika maswala ya ufuatiliaji na tathmini
ya mradi ndani ya asasi.

4.1 ununuzi wa samani za ofisi umefanyika ikiwa ni pamoja na kulipa posho za kila mwezi
kwa baadhi ya watendaji wa ofisi



1.1 Kuendesha mafunzo ya siku 3 kwa wanachama 20 na viongozi 6 jumla yao 26 kutoka
asasi ya WIDEK kuhusu usimamizi wa miradi na fedha katika asasi

1.2 Kutengeneza muongozo wa sera za fedha, uhasibu na taratibu za manunuzi ya asasi.

2.1 Kufanya mafunzo (retreat) ya siku 5 ili kuwawezesha wanachama, viongozi na wadau
kupata mwelekeo wa mpango mkakati (identifying strategic direction issues) na kuandaa
mpango mkakati.

3.1 Kuendesha mafunzo ya siku 3 kwa viongozi 6 na wanachama 20 jumla yao 26 juu ya
uendeshaji wa asasi na majukumu ya viongozi na wanachama katika usimamizi wa
shughuli za asasi ifikapo Augost 2011.

3.2 Kufanya ufuatiliaji na tathmini ili kuweza kubaini mapungufu ya mradi ifikapo septemba
2011.

4.1 Kulipia gharama za shughuli za utawala na uendeshaji wa ofisi


1.1. Mafunzo ya siku 3 yamefanyika kwa viongozi 6 na wanachama 20 wa WIDEK kwenye
ukumbi Red Cross Kigoma, kuanzia tarehe 02 - 04/8/2011 Masuala yaliyoshughulikiwa
ni kuwajengea uwezo wanachama na viongozi kuhusu usimamizi wa miradi na fedha
katika asasi, Kutengeneza draft ya kwanza ya muongozo wa sera za fedha, na taratibu
za manunuzi ya asasi.

2.1. Yamefanyika mafunzo ya siku 5 kwa wanachama, na viongozi wa WIDEK, wadau
kutoka asasi za Women Promotion Center, Zuia umasikini na maradhi kwa mama na
mtoto na Halmashauri ya manispaa Kigoma/Ujiji jumla yao 26, kuhusu uandaaji wa
mpango mkakati wa asasi na namna ya utekelezaji wake na Kutengeneza draft ya
kwanza ya mpango mkakati huo. Mafunzo yamefanyika katika ukumbi wa Red Cross
Kigoma kati ya tarehe 14 - 18/08/2011.

3.1. Mafunzo ya siku 3 yamefanyika kwa viongozi 6 na wanachama 20 wa WIDEK kwenye
ukumbi Red Cross Kigoma, kuanzia tarehe 10 - 12/08/2011 Masuala yaliyoshughulikiwa
ni uendeshaji wa asasi na majukumu ya viongozi na wanachama katika usimamizi wa
shughuli za asasi

3.2. Ilifanyika tathmini ya mradi kwa muda wa siku1 tarehe 21/09/2011 katika ukumbi wa
Women Promotion Centre kwa wanachama wa WIDEK, wadau kutoka asasi za WPC
na ZUMAM, jumla yao 10. Masuala yaliyoshughulikiwa ni kufanya ufuatiliaji na tathmini
ili kuweza kubaini mapungufu katika utekelezaji wa mradi.

4.1. Maswala yaliyoshughulikiwa ni kulipa posho za kila mwezi (kwa muda wa miezi 3) kwa
Mratibu na Muhasibu, kulipa kodi ya pango la ofisi kwa miezi 6, kununua viti 4 vya
plastiki, kununua meza mbili kubwa (moja ya Mwenyekiti na meza ya kompyuta), kiti 1
cha Mwenyekiti, kabati 1 ya kutunzia faili na ununuzi wa shajala (stationary)








Tofauti iliyojitokeza ni mabadiliko ya muda wa utekelezaji kutofautiana na mpango kazi, na hii imetokana na kuchelewa kwa fedha kutoka kwa mfadhili (FCS).
1.1. TSHS. 1,602,900
2.1. TSHS. 2,502,900
3.1. TSHS. 1,554,900
3.2. TSHS. 421,000
4.1. TSHS. 1,418,300

Mafanikio au Matunda ya Mradi

1.1. Wanachama 20 na viongozi 6 Jumla yao 26 wa asasi wameelewa uandishi na
usimamiaji wa miradi na fedha, kuandaa muongozo wa sera ya fedha, na wameanza
kuandika miradi na kuituma kwa wafadhiri.

2.1. Mpango mkakati wa asasi umeandaliwa.

3.1 Viongozi 6 na wanachama 20 jumla yao 26 wa asasi wameelewa uendeshaji wa asasi,
majukumu ya viongozi na wanachama katika usimamizi wa shughuli za asasi.

3.2 Wanachama na viongozi jumla 10 wameshiriki katika maswala ya ufuatiliaji na tathmini ya
mradi ndani ya asasi.

4.1 Ununuzi wa samani za ofisi umefanyika ikiwa ni pamoja na kulipa posho za kila mwezi
kwa baadhi ya watendaji wa ofisi.
1.1. Taratibu za utunzaji wa kumbukumbu za fedha unazingatiwa na vitabu husika vinatumika
(Analysisi Cash book, Ledger book, Hati za malipo na kuombea fedha na kitabu cha
risiti)
1.2. Wanachama na viongozi wamekuwa na uelewa kuhusu kuandaa maandiko ya miradi, na
miradi miwili imeandaliwa na kutumwa kwa wafadhili.

2.1. Uelewa kuhusu mpango mkakati umeongezeka kwa wanachama na viongozi wa asasi.

3.1. Hakuna mgongano/ muingiliano wa majukumu kati ya viongozi na wanachama katika
asasi.Bidii na ari ya kufanya kazi imeongezeka kwa wanachama na viongozi.

3.2. Wanachama na viongozi wamekuwa na uelewa na kujua umuhimu wa ufuatiliaji na
kufanya tathmini katika shughuli mbalimbali za asasi.

4.1. Asasi imeweza kulipia kodi ya pango la ofisi, ofisi sasa ina samani za kutosha, Viti 4
vya plastiki, Meza mbili kubwa (moja ya Mwenyekiti na meza ya kompyuta), Kiti 1 cha
Mwenyekiti, Kabati 1 ya kutunzia faili na Shajala (Stationary), pia ofisi imeweza kuajili
watendaji 2 wanaolipwa posho Mratibu na Muhasibu.



1.1. Utekelezaji wa shughuli ulichelewa kuanza kwa muda wa mwezi mmoja tofauti na
mpango kazi ulivyokuwa ukielekeza.

2.1. Shughuli ilianza mwezi wa nane badala ya mwezi wa saba kama ilivyokuwa imepangwa
kwenye mpango kazi ambapo ilipelekea shughuli zote kusogea mbele.

3.1. Shughuli ilianza mwezi wa nane badala ya mwezi wa saba kama ilivyokuwa imepangwa
kwenye mpango kazi ambapo ilipelekea shughuli zote kusogea mbele.

3.2. Shughuli ilifanyika mwezi wa tisa badala ya mwezi wa nane kama ilivyokuwa
imepangwa kwenye mpango kazi ambapo ilipelekea shughuli zote kusogea mbele.

4.1. Ofisi imekuwa na hadhi na muonekano wa kiofisi, utendaji wa kazi za ofisi na
mahudhurio vimeongezeka.





1.1. Kuchelewa kwa fedha kutumwa toka kwa mfadhili (FCS)
2.1. Fedha kuchelewa kutumwa kutoka kwa mfadhili (FCS)
3.1. Fedha kuchelewa kutumwa kutoka kwa mfadhili (FCS)
3.2. Fedha kuchelewa kutumwa kutoka kwa mfadhili (FCS)
4.1. Kabla ya mradi ofisi haikuwa na samani za kutosha na hakuna mtendaji aliyekuwa
akilipwa posho, hivyo kushindwa kuwa na Muhasibu, na baadhi ya watendaji kutokuwa
na ari ya kufika ofisini mara kwa mara.








Mambo Mliyojifunza

Maelezo
Kushirikiana na wadau wengine katika utekelezaji wa mradi ni muhimu kwani kunaleta upana wa uelewa wa mambo mbalimbali.

Mafunzo ya kujengewa uwezo katika asasi ni muhimu sana katika uendeshaji wa asasi, yanasaidia kuboresha ufanisi na utendaji wa asasi ikiwa ni pamoja na viongozi na wanachama kila upande kujua wajibu wake.

Changamoto

ChangamotoNamna mlivyokabiliana nazo
Kutumika kwa lugha ya kingereza hasa wakati wa mafunzo ya usimamizi wa fedha za asasi (wawezeshaji kuandaa vitini kwa lugha ya kiingereza).Ilibidi wawezeshaji kutumia sana lugha ya kiswahili katika kufundisha.
Kupanda kwa baadhi ya bei za vitu tofauti na makadirio ya bajeti iliyopitishwa.Tulilazimika eidha kupunguza idadi ya vitu au kununua tofauti na vilivyokusudiwa ili kulinda kutovuka bajeti iliyopangwa.

Mahusiano

WadauNamna mlivyoshirikiana nayo
Halmashauri ya Manispaa Kigoma/UjijiKushiriki katika mafunzo ya kuandaa mpango mkakati

Halmashauri ya wilaya KibondoKutoa wawezeshaji katika mafunzo haya
Serikali ya mtaa - KilimahewaUshiriki katika mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini

Mipango ya Baadae

(Hakuna jibu)

Walengwa Waliofikiwa

    Walengwa wa moja kwa mojaWalengwa wasio wa moja kwa moja
Wajane na WaganeWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watu wanaoishi na VVU/UKIMWIWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
WazeeWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watoto YatimaWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
WatotoWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watu wenye UlemavuWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
VijanaWanawake(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Wanaume(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Jumla(Hakuna jibu)(Hakuna jibu)
Watu wengineWanawake25(Hakuna jibu)
Wanaume01(Hakuna jibu)
Jumla26(Hakuna jibu)
(Hakuna jibu)

Matukio Mliyoyahudhuria

Aina ya TukioLiniMambo uliyojifunzaHatua zilizochukuliwa
Mafunzo ya usimamizi wa Ruzuku (MYG)20 – 25 Juni 2011- Jinsi ya
kusimamia
utekelezaji wa
miradi

- Namna ya
kuandaa na
kuandika vitabu
vya fedha

- Uandaaji wa
taarifa za fedha

- Utoaji wa taarifa
za utekelezaji wa
miradi

- Ufuatiliaji na
Tathmini

Kusaini mkataba kati WIDEK na The Foundation for Civil Society kwa ajili ya kupatiwa Ruzuku.

Viambatanisho

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.