Fungua
Tanzania Women of Action(Tawa)

Tanzania Women of Action(Tawa)

Dar es salaam, Tanzania

MAMBO TULIYOJUMUISHA KWA WIKI HII.

kwanza kabisa tunaishukuru serikali kwa kumaliza mgomo wa ma daktari uliodumu takribani wiki tatu.Hii imetufundisha kuwa katika kudai haki ni lazima uchukue hatua zinazokubalika ili chombo husika kiweze kutambua suala husika 

tumeshuhudia watu walioathirika kwa kiasi kikubwa ni wanawake na watoto,kwani asilimia kubwa ya watoto wanaolazwa ni akina mama ndio wanao wajibika kuwauguza na akina baba wakiwa katika shughuli zao nyingine .Hivyo tunaiomba serikali kushughulikia migogoro  mapema baina yake na makundi mbali mbali ili kunusuru akina mama na watoto.

  Migomo ni dalili ya ukosefu wa haki na usawa wa mgawanyo wa rasilimali tulizonazo,kwa hali hiyo asasi za kijamii na wanaharakati mbali mbali wanatakiwa kufanya kazi ya kuelimisha wananchi na jamii kwa ujumla ili kufahamu haki na usawa wa rasilimali tulizonazo pamoja na mgawanyo wake uko vipi.

11 Februari, 2012
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Maoni (3)

Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu kinondoni) alisema:
Tunawapongeza wanaharakati waliojitokeza kuonyesha hali ya kujali kwa kuandamana kuishinikiza serikali kumaliza mgomo wa madaktari ,hii imeonyesha kuwa kati ya wanaharakati waliojitokeza ni wanawake TAMWA, LHRC.TGNP na wengine ambao wameonyesha kuguswa kwa matatizo mbali mbali yaliyojitokeza wakati wa sakata hilo. Hii imeonyesha kuwa wanawake ni jasiri na tunaweza pia.
11 Februari, 2012
Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu kinondoni) alisema:
Tunaomba makundi mengine ya wanawake kuiga mfano wa bi Kijo Simba, na Annanilea Nkya kwa ujasiri waliouonyesha pia upendo na kujali maisha ya watanzania wengine.
11 Februari, 2012
Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu kinondoni) alisema:
Wanawake tujengeane uwezo na tuwe na nguvu ya pamoja ili tutetee jamii ya watanzania .
11 Februari, 2012

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.