Parts of this page are in Swahili. Edit translations
Interview 4
1.Unaishi eneo gani?!
Keko mwanga 'A'
2.Mtaa wako unahitaji kitu gani sana sana?!
- Kutengeneza mifereji,kudhibiti na kubomoa watu waliojenga bila mpango maalumu.
- Tuliopo mabondeni tuhamishwe maeneo bora zaidi.
3.Mafuriko yameleta athari gani kwenye nyumba unayoishi na vitu vyako?!
Mali zangu zote za ndani zimepotea,vifaa vya kazi yangu kama mashine ya kuranda zimepotea zenye zaidi ya thamani ya Mil 2 na laki tano.
4.Mafuriko yameleta athari gani kwenye maisha yako ya kila siku?!
- Yameniathiri kiuchumi maana vifaa vyangu vya kazi vimeharibika hivyo siwezi kufanya kazi yangu inayoniingizia hela.
- Magonjwa kama Malaria,kuharisha na tumbo kuumwa kwa mimi na familia yangu.
- Choo changu kuharibika.
5.Vyanzo bora vya maji vimepata athari gani kutokana na mafuriko?!
Tunakosa maji ya kunywa kutokana na maji yetu ya kisima kuchanganyika na maji taka,hivyo maji tunayotumia si salama kwa matumizi bora kwa afya ya binadamu.
6.Kama una kazi,inakuchukua muda gani kutoka nyumbani mpaka eneo lako la kazi?!
Hainichukui muda wowote maana ofisi yangu ilikua hapohapo nyumbani.
January 31, 2012