Interview 3
1.Unaishi eneo gani?!
Magulumbasi 'B'
2.Mtaa wako unahitaji kitu gani sana sana?!
- Kuvunjwe nyumba ambazo zimejengwa kando ya mtaro,kutengenezwe njia ya maji kutoka keko darajani mpaka bahari ya hindi.
- Kutengenezwe njia ndogo ndogo zitazoweza kupitisha maji kwa urahisi na mitaro izibuliwe mara kwa mara.
3.Mafuriko yameleta athari gani kwenye nyumba unayoishi na vitu vyako?!
Tv na redio ndivyo vimeharibika,vingine niliwahi kuhamisha kutoka ndani ya nyumba.
4.Mafuriko yameleta athari gani kwenye Maisha yako ya kila siku?!
Magonjwa kama Malaria,Kuharisha,kutokana na maji taka mbu hawazuiliki hata kwa matumizi ya chandalua.
5.Vyanzo bora vya maji vimepata athari gani kutokana na mafuriko?!
Bomba lilipasuka hivyo hatuna kabisa maji ya kutumia,inatubidi kwenda kuchota maji kwenye mabomba ya watu na kutugharimu hela kuyapata maji hayo.
6.Kama una kazi,inakuchukua muda gani kutoka nyumbani kwako mpaka eneo lako la kazi?!
Sina muda maalumu maana biashara yangu ni ya kuzunguka kwa watu na kukopesha bidhaa ninazouza.