Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

 

PROGRAMU YA YOUTH INFORMATION CENTRE YAJA TANZANIA,DAR-ES-SALAAM IKIWA SEHEMU YA MAJARIBIO.


Wizara ya habari,utamaduni,vijana na michezo imepokea na kukubali mpango wa taarifa na habari kwa vijana utakaojulikana kama Youth information Centre.Mpango huu uliasisiwa ama kupendekezwa na bi Joyce Shahidi mkurugenzi msaafu wa Idara ya vijana ya wizara hiyo kwa alipokuwa kwenye kikao cha wadau nchini kenya miaka kama miwili iliyopita.

Programu hii inalengo la kurahisisha upatikanaji wa habari zitakazohusu nyanja mbalimbali za ustawi wa  vijana hasa ukizingatiwa kuwa vijana ndio wahanga wakubwa wa changamoto nyingi za maisha.Hivyo kituo cha habari cha vijana kitakuwa kinajibu maswali ya vijana katika changamoto mbalimbali watakazo kuwa wanakabiliana nazo.

 

Kituo katika hatua za awali kitakuwa ni cha mfano kwa kuanzia katika wilaya za Temeke,Ilala na Kinondoni na kutakuwa na kituo cha taifa cha habari kwa vijana vyote vitakuwa chini ya wizara na Manispaa husika.

Wizara imeunda timu ya watu 7 kushughulikia mchakato wa uundwaji wa kituo hicho na kwa pamoja na wadau walihojiwa imeundwa timu ya watu 14 itakayotoa maoni juu ya namna gani kituo hicho kitakavyochukua sura ya vijana wa kitanzania.

TEYODEN imetoa uwakilishi wa vijana wawili katika timu hiyo ya mchakato wa maoni na kuchagiza uundwaji wa kituo hicho.

Vijana tuamke na kufuatilia juu ya fulsa hii muhimu kwetu.

 

Wadau 12 wa timu ya Uundwaji wa kituo cha Habari cha vijana wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa katika Hotel ya Peacock tarehe 12/7/2012.

Wadau wa timu ya Uundwaji wa kituo cha Habari cha vijana wakiwa katika mjadala wa pamoja wa namna ya kuanzisha kituo cha habari cha vijana katika Hotel ya Peacock tarehe 13/7/2012.


July 16, 2012
« Previous Next »

Comments (2)

Gabriel Samalu (magu-mwanza) said:
nimefurahi kwa harakati hii ya vijana mimi kama m/k wa cbo ya KIKUNDI CHA AMKENI VIJANA ya magu napenda kutoa ushirikiano kwa kushirikiana nanyi kwa namna niwezayo
July 17, 2012
Ismael mnikite (Temeke) said:
Binafsi hili ni jambo jema sana hasa kwa vija walio nje wa mfumo rasmi,na kwa dhati kabisa serikali yetu kwa hili inastahili pongezi na napenda niwapongeze vijana wawakilishi toka mtandao wa vijana Temeke kwani dhamana hii ni kubwa na sina chembe ya shaka nyinyi ni vijana mahili na makini katika masuala nyeti kama jambo hili na Imani yangu mna uzoefu wa kutosha na mmestahili kutuwakilisha sisi vijana hasa tulio pembezoni ya fursa mbalimbali ikiwemo hili ya uhakika wa kupata habari na taarifa muhimu zinazotuhusu na kutugusa katika maisha yetu ya kila siku.
August 25, 2012

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.