Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

WASICHANA WALIOZAA CHINI YA UMRI WA MIAKA 20 NA AMBAO WAPO KATIKA MAZINGIRA HATARISHI WAPATA NAFASI NYINGINE YA KUPEWA MAFUNZO NA MITAJI ILI WAWEZE KUJIENDESHA KIMAISHA.

TEYODEN imefanya shughuli ya utambuzi wa wasichana  walio katika mazingira hatarishi ambao pia wamezaa chini ya miaka 20 ili waweze kuwa wanufaika wa mradi wa mwaka mmoja utakao kuwa unawawezesha kusimama upya kama watu wengine katika jamii.Mradi huu unaoendelezwa baada ya kutekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja hapo 2011-2012.Moja kati ya matunda ya mradi kwa kipindi cha utekelezaji cha 2011-2012 ni kuwezesha wasichana (kinamama wadogo) 20 kuwa na miradi ya kiuchumi iliyochangia kujiwekea akiba ya sh 1,200,000 benki inayosubili kujenga uwezo wa wasichana wengine zaidi.

Wasichana (wamama wadogo) 8 na mratibu wa mradi wameuhudhuria mafunzo ya siku  6 jijini Arusha kupata mafunzo zaidi ya namna ya kukabiliana na changamoto zilizojitokeza katika kutekelezaji wa mradi huu kwa kipindi kilichopita.

Katika kipindi cha siku 10 zijazo wasichana 60 (20 wanaoendelea na 40 wapya) watapata nafasi ya kuwezesha mafunzo ya stadi za maisha na stadi za ujasiliamali kabla ya kupewa mitaji kwaajili ya kuanzisha  na kuendeleza biashara walizo/watakazoziibua katika maeneo yao kama hatua/shughuli  moja wapo ya mradi huu.

Katika kipindi cha utekelezaji cha 2013-2014 mradi huu utaendelea katika kata za Azimio,Mtoni na Kibada na unategemea kuwanufaisha wasichana wa waliofanya vizuri katika kipindi kilichopita na wasichana wengine wapya.

"Nawakaribisha sana wasichana ambao wamezaa chini ya miaka 20 kujiandikisha kwa wingi kwa watendaji wa mitaa na kata katika zilizotajwa hapo juu ili waweze kusailiwa na kuandikishwa katika orodha ya wanufaika wa mradi" anasema mratibu wa mradi bwana Yusuph Kutegwa.Walimu wa wasichana waliochaguliwa na wasichana wenyewe wakiwa kwenye mafunzo ya uongozi na uwezeshaji,Ukumbi wa Azimio la Arusha jijini Arusha.

 

TEYODEN NA TRA MAKAO MAKUU WAFANYA MAFUNZO KWA VIJANA 100, KUHAM ASISHA URASIMISHAJI WA BIASHARA NA ULIPAJI WA KODI.

Tunasema kuwa hakuna wakati ambao vijana wanahitaji kuongeza juhudi za kujiajiri wenyewe kuliko kipindi hiki.Vijana wengi sasa wameanzisha biashara ili waweze kukidhi mahitaji ya kila siku ya maisha.

Upo umuhimu mkubwa wa vijana kupata elimu mbalimbali ili waweze kundesha biashara zao vizuri ikiwemo elimu ya ujasiriamali,stadi za masha,umuhimu wa usajili wa biashara na ulipaji wa kodi.Mafunzo haya huwafanya waweze kufanya biashara kwa utaratibu na kufuata sheria na kupunguza hatari za kuchukuliwa kama wanavunja sheria na kuhadhibiwa.

Mtandao wa vijana Manispaa ya Temeke(TEYODEN) na Tanzania Revenue Athority(TRA) tumeshirikiana kuwezesha mafunzo ya siku 1 kwa vijana 100 wafanyabiashara kutoka kata 30 za Manispaa ya Temeke.Mafunzo haya yamefanyika katika ukumbi wa Chuo cha utalii,kilichopo Tandika,Temeke Dar-es-salaam.Pamoja na mambo mengine vijana walijifunza umuhimu wa kusajili biashara,umuhimu wa kulipa kodi na elimu ya ujasiriamali.

TRA na TEYODEN tutaendelea kuelimisha wafanyabiashara vijana ndani na nje ya Temeke ili kuwawezesha kufanya biashara kwa uhakika na kuleta tija kwao na kwa vijana wengine.

 

MAFUNZO YA UJASIRIAMALI YANAYOENDESHWA NA MTANDAO WA VIJANA (TEYODEN) YAENDELEA KATIKA WIKI YA TATU.

Sasa imeshafikia wiki ya tatu toka mafunzo ya anzisha na kuza wazo lako la biashara yanayoendeshwa na TEYODEN hapa,Temeke kwa kushirikiana na mwezeshaji kutoka I.L.O yanayosimamiwa na asasi ya Restless Tanzania.

Mafunzo haya yanachukua wastani wa wiki moja kwa kila kundi la vijana 30.Mpaka sasa tumefikia vijana 60 kutoka katika kata 3 ambazo ni Chang’ombe,Keko na kata ya  Kijichi.Shabaha yetu hasa ni kufikia vijana 300 kutoka katika kata zote 30 za manispaa ya Temeke,wafikirie vyema mawazo yao ya biashara,wayakuze na yawezeshe  ajira kwao na kwa vijana wengine.

Tathmini ndogo tuliyofanya kwa walengwa waliopatiwa mafunzo haya,wanasema kuwa, hakujawahi kufanyika kwa mafunzo mazuri ya ujasiriamali kama haya ya wakati huu.Hivyo wanawashauri vijana wengine wa Manispaa ya Temeke kujitokeza na kutumia fulsa hii.

 Utaratibu wa kuomba nafasi hii ya kuwa mmoja wa vijana 300 watakaowezeshwa kupata nafasi ya kuelimishwa ni pamoja na kuchukua fomu,kuijaza na kuirudisha katika ofisi za TEYODEN zilizopo Mtaa wa Bora,karibu na TRA,Katika jengo la Afisa Mtendaji wa kata ya Chang’ombe tunawakaribisha sana vijana wote.

 Note that: Maendeleo ya mtu huletwa na mtu mwenyewe na si vinginevyo.

Mafunzo ya project management Naivasha Kenya yatakuwa chachu ya mabadiliko ya vijana kuelekea ujasiriamali na utengenezaji ajira binafsi kwa vijana.

Siku 8 za mafunzo ya uendeshaji wa miradi yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na ILO  y2y fund pamoja na UNHABITAT youth fund zimebadilisha mtazamo wa mameneja 10 kutoka Tanzania.Mameneja hao kwa sasa, wanafikiria kuboresha miradi 10  ambayo ILO wameichagua kati ya miradi 103 iliyoombwa katika mfuko huo wa vijana kwa mwaka 2012.miradi ya mwaka huu imegusia maeneo ya taka ni pato,ulimaji wa mboga mboga kwa njia za kiasili,uongezaji wa thamani katika mazao ya chikichi,uvunaji wa asali,uboreshaji wa sabuni za maji na utengezaji wa batiki,uboreshaji wa bidhaa za ngozi,new chips vending,uboreshaji wa mazao ya muhogo kutengeneza biskuti.

Mameneja watakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa miradi inakwenda vizuri na kutoa ajira kwa vijana nchini Tanzania.

Mafunzo yalikusanya mameneja wa miradi kutoka nchi za Togo.benin,zambia,kenya uganda,malawi.kongo,Tanzania,mauritius,misri na nyingine nyingi.

Hata hivyo mifuko hiyo itaendeleo kuwezesha vijana barani afrika na kwingineko kuwawezesha vijana kuongeza ajira binafsi kwa kuwa tatizo la ajira rasmi na zenye tija limekuwa ni kubwa sana.


 

MABINTI KATIKA KATA ZA AZIMIO, CHARAMBE NA MBAGALA WAPATA MRADI MPYA WA KUWAJENGEA UWEZO.

Mradi mpya wa kuwajengea uwezo mabinti wa umri kati 15-19 umezinduliwa katika viwanja vya Zakhiem.Mradi huu ambao unategemea kutekelezwa kwa ubia kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na Restless kwa kushirikiana kwa karibu kati ya UNICEF na TACAIDS utatekelezwa katika kata za Azimio,Charambe na Mbagala walengwa wakiwa ni wasichana wa umri wa kati ya miaka 15-19 kutoka kata husika.

Mradi kama huu ulifanywa na Mtandao wa Maendeleo ya Vijana Manispaa ya Temeke kwa ushirikiano na Tamasha na ufadhili wa Population Council ukihusisha kata za Azimio,Mtoni,Vijibweni na Kibada.

 Akitoa maelezo Mwenyekiti mtendaji wa TACAIDS bi Fatuma Mrisho aliwaasa wanaume kutoa wanyanyasa wasichana kwa kuwa na haki sawa kama wanaume.Alilisisitiza kuwa hali ni mbaya kwa kuwa maambukizi ni makubwa sana upande wa wasichana.”Karibu robo tatu za walioathirika na maamukizi ya V.V.U ni wasichana,mbaya zaidi karibu asilimia 30 ya wanawake waliowahi kufanya ngono wanaona sawa kufanya ngono kwa kulazimishwa”alisema mama Mrisho.

 Katika nasaha zake Miss Tanzania wa mwaka 2004 Bi Faraja Kota aliwapa moyo wasichana na kuwataka kujitambua na kuwa na dira katika maisha kwa kuwa kila kitu kinawezekana kwao.Aliwashauri wasichana kuwa ngangari na kamwe wasikubali kuchakachuliwa.Faraja alimalizia kwa kusema hata yeye amepata nafasi ya ukamishna wa Tume ya kudhibiti Ukimwi kwa sababu aliona anaweza hivyo wasichana wasikate tamaa na kujirahisisha.

 Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke bwana Mzirai aliwakaribisha kwa roho kunjufu watekelezaji wa mradi huo Restless development na aliwataka kutumia uzoefu na taaluma za watalaam waliopo katika Manispaa ya Temeke na kata za mradi ili mradi huo uweze kufanya vizuri na kutoa matokeo kama inavyotarajiwa.

Mradi wa Mabinti shika hatamu unategemea kuanza muda wowote baada ya uzinduzi na kwamba wasichana katika kata 3 za mradi wakae tayari kuweza kushiriki katika hatua mablimbali za utekelezaji wake.

  

 

International Youth day emphasizes building a better world: Partnering with Youth

“To unleash the power of young people, we need to partner with them”- UN SG – Ban Ki-moon

Dar es Salaam - The UN system in the context of Delivering as One in Tanzania collaborated with the government of Tanzania, youth organizations and partner NGOs to commemorate the International Youth Day (IYD) on 11 August at Mwembe Yanga grounds in Temeke district.

The IYD is celebrated internationally each year on 12 August.  The theme for this year’s observance was “Building a Better World: Partnering with Youth”.  It emphasizes a global call to action for young men and women, as well as other stakeholders around the world, to develop and engage in partnerships with and for youth towards building a better world.

In Tanzania just like in other countries, IYD provides an important opportunity to build upon the priorities of the government on youth agenda, to share information with youth as well as respond to calls from youth organizations. This is the right opportunity to strengthen partnerships and collaboration with young people, especially in the areas of employment, entrepreneurship, political inclusion, and citizenship, protection of rights, education opportunities and issues pertaining to sexual reproductive health.

In his statement, the UN Secretary General, Ban Ki-moon emphasized and called on strengthening of partnership with young people. He held in part that the UN “calls on governments, the private sector, civil society and academia to open doors for young people and strengthen partnerships with the youth-led organizations. Youth can determine whether this era moves toward greater peril or more positive change. Without urgent measures, we risk creating a “lost generation” of squandered talent”. He commented.

The Guest of Honor at the ceremony was the Minister of Information, Youth, Culture and Sports, Dr. Fenella Mukangara. In a speech read on her behalf she said, “Youth development as crosscutting starts from the family, community, national and international levels, therefore the Ministry calls for a concerted effort to create an enabling environment for partnering with youth”.

The United Nations in Tanzania was represented by the UNFPA Acting Representative in the country, Ms. Mariam Khan. She urged the government and the society to commit to incorporating youth as partners and ensure that youth participate in decision making at every level in their families, in communities and within the nation. “Young people need to have a voice in matters that concern them and their communities”, Khan stated during the 2012 International Youth Day.

The event t highlighted key issues specific to Tanzania youth under five thematic areas including HIV prevention. In Tanzania, Youth aged 15 – 19 account for 60% of all new HIV infections, 2.4% of adults aged 15 – 24 are infected with HIV  this is according to the 2008, Tanzania HIV and Malaria Indicator Survey.  It also presents that young women aged 15 – 10 are four times more likely to be infected than their male counterparts. The key message at the event was “Turning the tide together, reducing the vulnerability of women and girls to HIV”.

The second key message was on Gender based violence. The concern was on prevalence of Female Genital Mutilation or circumcision-FGM/C .  Trends show a slight decline over the past few years, from 18% in 1996 to 15% in 2010. Overall, 11 % of women aged 20 – 24 and 75 of girls aged 15 – 19 have undergone FGM/C.  The key message advocated for was  “FGM/C violates the right to the highest attainable standard of health and to physical and mental integrity of women and girls”. Or “It is possible to end FGM/C without giving up meaningful aspects of culture – Stand up against FGM/C”

The third key message was on the ratification of the Africa Youth Charter reservation: In February of 2012, The Government of Tanzania ratified the Africa Youth Charter with a reservation on Article 13.4h which states “ensure, where applicable, that girls and young women who become pregnant or married before completing their education shall have the opportunity to continue their education”. The key message:  “Pregnant or not all girls have the right to be in school”

The fourth key message was on the upcoming Census which is scheduled to take place on August 26th 2012, the census will provide age and sex disaggregated data for improved policy formulation and development planning at national, sub-national and sectoral levels. The key message for the youth is that they should avail themselves for the census since “Good data is the foundation to economic development – stand up and be counted for a better tomorrow”.

The fifth message was on Family planning. Almost one quarter of women aged 15 – 19 are either pregnant with their first child or are already mothers.  Family planning alone reduces one third of maternal deaths, which is the leading cause of death among pregnant adolescents’ girls, especially from poor households. The unmet need for family planning stands at 16% for currently married women aged 15 – 19 and 24.4% for currently married women aged 20 – 24. The key message shared with the youth was  “Plan your life, Plan your future”.

To celebrate the day, two football matches (male and female teams) were organized; voluntary  HIV counseling and testing services; family planning information and services; entertainment from several youth organizations; and an educational exhibition  organized by UNIC’s Reference Assistant Harriet Macha was open to the young people.

Prior to 12 August, youth visited media houses as part of  a media campaign to promote awareness on the key messages and inform the youth about their International Youth Day 2012 and the events that would take place. Media houses that were visited included TBC’s Busati discussion panel programme, Clouds interviews and discussions, Choicefm panel discussion and Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) radios; TBC and Star TV stations for discussion programmes.

This event was organized by a committee comprising of UNESCO, ILO, UNIC,UNFPA, AMREF, Tanzania Commission for AIDS (TACAIDS), Ministry of Health and Social Welfare, Ministry of Information, Youth , Sports and culture, Children’s Dignity Forum, Temeke Youth Development Network, Tanzania Youth Coalition and Youth of the United Nations Association.

International Youth Day

Start Date: 12 August 2012


"Building a Better World: Partnering with Youth"
This year's International Youth Day (IYD) event was held on the 11th of August 2012 at the Mwembe Yanga Grounds in Temeke District. The event was a collaboration between the Ministry of Information, Youth Sports and Culture and UNFPA with support from other organizations including ILO, UNIC, UNESCO, AMREF, UMATI, TYC, CDF, UNFPA-YAP and Temeke Youth Development Network (TeYoDeN). Activities held on the day included 2 Soccer matches between 4 football teams, 2 female teams and 2 male teams. Supporting activities such as HIV Counseling, testing and Family planning counseling and services were also provided during the event.

The event aimed to highlight key issues specific to Tanzania youth under five thematic areas for education and awareness including; HIV/AIDS prevention, Family planning, Female Genital Mutilation/Cutting, 2012 Census and the African Youth Charter reservation on the article allowing equal access to education for young girls who become pregnant while in school. Over 1000 youths from the three districts of Dar es Salaam attended the event and around 600 persons were reached through IEC materials as well as counseling and testing services.

In her closing remarks, the United Nations Population Fund Acting Representative, Mariam Khan, urged the government and the society to commit to making youth partners to development and to ensuring that youth participate in decision making at all levels. "young people need to have a voice in matters that concern them and their communities.". Khan commented
International Youth Day is celebrated each year on 12 August to encourage young men and women, as well as other stakeholders around the world to develop and engage in partnerships with and for youth towards building a better world. The theme of the 2012 celebration was "Building a Better World:

WIKI YA VIJANA YAISHA SALAMA MKOANI SHINYANGA HUKU WILAYA YA TEMEKE IKIIBUKA MSHINDI WA KITAIFA.

Maadhimisho ya wiki ya vijana ya mwaka 2012 yamefanyika mkoani shinyanga kwa kuhusisha halmashauri mbalimbali za wikaya na mikoa hapa Tanzania.Maadhimisho haya hufanyika kila mwaka kama wiki ya vijana ya kutathmini mipango ya vijana na kuweka vipaombele kwaajili ya maendeleo ya vijana hapa nchini Tanzania.

Wiki hii huwa inaenda sambamba na maadhimisho ya kumuenzi baba wa taifa ambaye alifariki dunia siku ya terehe 14/10/200.Ili kuenzi mambo mazuri ambayo ameyaacha shughuli mbalimbali hufanywa ikiwemo mihadhara,makongamano maonyesho ya bidhaa na shughuli mbalimbali za sanaa.Yote ni kuenzi tu yale tu ambayo mwalimu nyerere ametuachia kama kumbukumbu ya kudumu.

Halmashauri ya manispaa ya Temeke iliwakilishwa na afisa maendeleo ya vijana na vijana 3 kwaajili ya maadhimisho hayo.TEYODEN iliwakilishwa na Maulidi Mziwanda mwenyekiti wa kituo cha vijana cha Azimio.