Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations
Asasi ya Mwanakwerekwe Environmental Ethics and Cultural Organization(MEECO) kwa kushirikiana na American Corner English Club,siku ya jumamosi ya tarehe 23 July 2011 itafanya dhiara ya kwenda Kijiji cha Unguja Ukuu, mkoa wa Kusini Unguja wilaya ya Kati.Dhiara hiyo itakuwa na malengo yafuatayo:
- Kuhamasisha Wanakijiji na Jamii ya Wazanzibar kwa ujumla umuhimu wa utunzaji,uhifadhi na Kulinda mazingira.
- Nafasi za Asasi zisizo za kiserikali katika jamii ya Mtanzania
- Umuhimu wa ushirikiano wa Asasi zisizo za kiserikali na uwongozi wa serikali za mitaa.
Shughuli zinazotarajiwa kufanyawa katika safari hiyo ni kama zifuatavyo:
- Kuonesha onesho la Mchezo wa Sarakasi litakalochezwa na Vijana wa Meeco Talent Group(MTG)
- Zoezi la upandaji wa miche ya mikoko
- Mashauriano kati ya Viongozi wa Kijiji na Wanadhiara.
Katika safari hii mgeni mualikwa anategemewa kuwa Mwakilishi wa jimbo la Amani. Na mshauri wa kigeni wa Asasi ya MEECO Miss. Katrina Demulling
Safari hiyo itakuwa saa 9:30 a.m
21 Nyakanga, 2011
Ibitekerezo (0)