Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

JIKWAMUE DEVELOPMENT ASSOCIATION-JIDA

jikwamue development Association ni Asasi ya Kiraia isiyotengeneza faida.

Asasi hii imeanzishwa mwaka 2010,na imepata Usajili tarehe 04/02/2011.chini ya sheria ya uanzishwaji wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Act 24/2002.

MAKAO MAKUU

Ofisi za Asasi hii zipo katika Kijiji cha Tambuu,Kata ya Lundi,Tarafa ya Matombo,Wilaya ya Morogoro Vijijini Mkoa wa Morogoro Tanzania.

JIKWAMUE DEV.ASS.

Asasi hii imeshafanya Mradi wa Kuwajengea Uwezo Wananchi wa Kata ya Lundi juu ya Ufuatiliaji wa Matumizi ya fedha za Umma (PETS) za Sekta ya Elimu na pia Mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti,Usimamizi wa Fedha za Umma na Utawala Bora kwa wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Lundi na Wajumbe wa Kamati za Shule zilizomo katika Kata ya Lundi

15 Ukuboza, 2012

Ibitekerezo (1)

mahinda saburi (Dar salaam) bavuzeko
JIKWAMUE DEVELOPMENT ASSOCIATION-JIDA YAJIKWAMUA
Asasi hii inastahili pongezi kubwa kwa mafanikio iliyoyapata tokea kuanzishwa kwake hadi mwaka 2014.
Mwaka 2013,JIDA,imefanikiwa kuandaa Mradi wa Mafunzo ya Ufuatiliaji wa Matumizi ya fedha za Umma za Sekta ya Elimu katika Kata 6 za Halmashauri ya Wilaya Morogoro Vijijini ambazo ni Mtombozi,Kisemu,Tawa,Konde,Mvuha na Selembala,
Mafunzo ambayo yaliwashirikisha Wanufaika 90,katika maana ya kwamba kila Kata iliwakilishwa na washiriki 15.
Mafunzo haya yaliandaliwa na JIDA kwa Ufadhili wa Foundation for Civil society,Mradi huu umeleta mafanikio makubwa sana kwa Jamii kwa kupata Elimu ya Mbinu au Stadi za Ufuatiliaji wa fedha za Umma,bali pia Jamii imetambua kuwa ni wajibu wao pia kuzisimamia fedha za Umma,ikiwemo kupanga,kusimamia,kufuatilia na kupima ubora wa bidhaa au huduma ilyotolewa.
Jikwamue Devel.Assoc.kupitia Mpango Mkakati wake ulioanza 2011 na kuishia 2013 imeweza kufanikiwa kutekeleza Azima yao ya kuwa na Ofisi kubwa na ya Kisasa,Kwa kuwa jida imejengga Heshima kubwa katika Jamii si ya Kijiji cha Tambuu Pekee na Nje ya Kata ya Lundi,hitajio hili la kuwa na Ofisi yetu wenyewe liliungwa Mkono na Wananchi wa Kijiji cha Tambuu na Viongozi wa Kijiji hicho akiwemo Mwenyekiti wa Kijiji hicho ndugu Hassani Dege,kwa mafanikio haya yote mimi ninawapongeza sana JIDA.
8 Nyakanga, 2014

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.