kwa kipindi chote hicho chuyodo ilikuwa na harakati za kuandika mradi kwa mara ya pili ikiwa ni miongoni mwa malengo yake kutokana na kutopata majibu ya mradi wa mwanzo ulioombwa na jumuia.
chuyodo imefanya tathmini ya muda mfupi kuhusiana na watuimiaji wa maktaba katika kipindi cha mwaka mmoja tangu kaanzishwa kwa huduma hiyo na kupata jumla ya watumiaji 328 wakiwemo wanawaje na wanaume pai rika tofauti na kuonyesha kuwa watumiaji wake wengi ni ni wanafunzi wa shule katika wilaya mzima wa mjini magharibi kuna asilimia 80 na aasilimia 20 kutoka wilaya nyengine tumeweza kuona matunda ya huduma hiyo na hadi hivi sasa tunaendelea vizura ijapokuwa tunakabiliwa na upotevu wa vitabu kwa watumiaji na eneo dogo la maktaba,pia tumo katika kutafuta wafadhili kwa kutununulia sehemu ili kukuza maktaba yetu
Mwezi wa 12 chuyodo iliweza kupata mashelfu na mafunzo ya siku mbili kutoka kwa Book Aid International kupitia mradi uliobwa na mjukiza ,hata hivyo tumeweza kusambaza barua za wito kwa masheha ,wabunge na wawakilshi wa shehia ya chumbuni
kutokana pia na kujishuhulisha na maktaba tumeweza kupokea vitabu vya fani mbalimbali kutoka maktaba kuu ya zanzibar ambavyo vinasaidia kwa kiasi kikubwa katika maktaba yetu.
pia tumeweza kuandika barua ya maombi katika idara ya mawasiliano na lesseni iliyipo mwanakwerekwe kwa ajili ya kuomba eneo la ardhi lililopo karibu na karakana kuu lakini kwa bahati mbaya tumekosa eneo hilo,hata hivyo tulifanya juhudi ya kuongea na mlezi wa jumuia ambae ni sheha wa shehi ana kutuambia tusubiri mpaka itakapo kamilika upitishaji wa waya za umeme unaotokea kidatu na kuangalia nafasi iliyowazi ili kupewa kwa kujengea ofisi
Vilevile vikao vya kila mwezi vimeweza kuamua kwamba tuombe kupitia mashirika ya nyumbani mfano ZANTEL,BENKkwa ajili ya kutununulia kiwanja kilichopo karibu na ofisi yetu kwa ajili ya kuboreshwa kwa jumuia yetu ambapo hadi hivi sasa tunasubibi majibu kutoka mashirika hayo
pia chuyodo imeweza kuandika mradi kipitia 'the foundation for civil sosiety' kwamara ya mwanzo kwa ajili ya kuijengea uwezo jumuia ya chuyodo ambapo hadi hivi sasa tunasubiri majibu kutoka kwao
mwezi waferbuary chuyodo iliweza kuunga uhusiano wa karibu na jumuia ya 'zanzibar youth foram iliyopo mlandege na kufanya mazungumzo mafupi katika ofisi ya chuyodo na mwenyekiti wa jumuia hiyo
mwezi huohuo chuyodo ilipata fomu ya maombi ya mafunzo kwenye shirika la FEES lililopo jijini dares salam kwa ajili ya mafunzo ya uongozi kwa muda wa mwaka mmoja ambapo mitihani ya majaribio ilifanyika umoja wa walemavu ambapo katika watu 30 kwa zanzibar walipatikana watu kumi akiwemo mwenyekiti wa chuyodoambae ni laila abdalla mansour na kutakiwa kuhudhuria mafunzo tarehe 30 na 31 katika jengo la fees upanga dares salam
tarehe 21/9/2011 chuyodo ili weza kufanya maamuzi ya kutafuta mwanasheriana mhasibu wa jumuia ambao walipatikana wote nawenye kiwango cha digirii, hata hivyo tumeweza kuchangishana kiasi cha pesa kwa ajili ya kuongeza vitabu vya jumuia,tulipata ugeni kutoka boook aid international ambao wapo canada kwa ajili ya kuangalia maktaba yetu ,tumezitembelea jumuia zilizokaribu na zetu mfano ZEDY,NGORC kwa ajili ya kutafuta ushiriiano kutokka kwao pia tumepata wanachama 18ambao woteni wanawake katika skuliza nasari baada ya kuwapa ushauri wa kuwataka wanafunzi wao waje kusoma katika maktabayetu na wao walitupa wazo la kutaka kushirikiana nasi kwa kuja kuwasomesha watoto hao kwa kutumia itabu vyetu