Injira

Ubusobanuro: Kinyarwanda (rw): User Content: WIRhU3kXXVEz8ZSXCOdz31vw:content

« Inyuma   ·   Ahakurikira »
Base (Icyongereza) Kinyarwanda

TANZANIA SOCIAL SUPPORT FOUNDATION
OFISI YA MKURUGENZI MKUU

TANGAZO
YAH: PUNGUZO LA ADA YA FOMU YA MAOMBI YA UFADHILI WA MASOMO YA ELIMU YA JUU KWA MWAKA 2017/2018


Hii ni kuutaarifu Umma wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba, baada ya kupokea maoni mbalimbali ya wadau kuhusu kushindwa kulipa ada ya maombi ya ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwa mwaka 2017/2018 kutoka TSSF, na kwa kuzingatia agizo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kutaka kushushwa kwa bei za maombi ya huduma za elimu ya juu kwa wanafunzi, na kwa kuzingatia misingi ya falsafa ya Shirika la TSSF ambayo ni ‘kutoa msaada kwa jamii’, Shirika la TSSF limepunguza rasmi kiasi cha malipo ya ada ya fomu ya maombi ya ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kutoka TSSF ambapo ada hiyo imepunguzwa kutoka Tshs. 50,000/= hadi Tshs. 20,000/= kuanzia leo siku ya Jumatano ya tarehe 30 Agosti 2017.
Aidha, wale ambao walikuwa wameshalipia Tshs. 50,000/= watarejeshewa Tshs. 30,000/= na kwamba utaratibu wa kudai kurejeshewa malipo tajwa hapo juu utafanyika baada ya mdai kuwasiliana na Shirika la TSSF kupitia Na. 0624 700 666 au kutuma ujumbe wa barua pepe kwenda kwa anwani ifuatayo; registry@tssf.or.tz
Sanjari na hilo Shirika la TSSF linawakumbusha waombaji wa ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwamba, mwisho wa kuomba ufadhili tajwa hapo juu ni tarehe 30 Septemba 2017.
Imetolewa na;


Donati Salla
MKURUGENZI MKUU – TSSF
30 Agosti 2017

(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe