Envaya

Translations: Kinyarwanda (rw): User Content: WI0004EE5657D25000041026:content

Base (Swahili) Kinyarwanda
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

CHAMA cha Waandishi wa Habari mkoa wa Mbeya(MBPC) kimepokeakwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mwanahabari mwenzetu,DannyMwakiteleko kilichosababishwa na ajali ya gari jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa MBPC mkoa wa Mbeya,Christopher Nyenyembeamekielezea kifo hicho kubwa ni pigo kubwa katika tasnia nzima ya habari hasakutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao marehemu enzi za uhai wake.

“Mwakiteleko alikuwa kamusi ya kitaaluma na kisima chafikra,mfumbuzi na mbunifu wa kazi mbalimbali za kihabari na aliweza kufanyakazi zake na kuibua vipaji vya waandishi wengine,hakika wengi hawatakujakumsahau”Alisema Nyenyembe.

Kwa kutambua uwezo aliokuwa nao kwa niaba ya waandishi wahabari mkoa wa Mbeya nachukua fursa hii kutoa pole za dhati kwa ndugu nafamilia yote ya Mwakiteleko bila kuwaacha marafiki zake wa karibu nawafanyakazi wa New Habari alikokuwa akifanya kazi kama Naibu Mhariri Mtendaji.

Kifo cha Mwakiteleko licha ya kuwa pigo kubwa katika tasniaya habari kwa namna moja au nyingine kimetuachia fumbo kubwa kwa wanaharakatiwengine waliokuwa wakitumia kazi zao kupiga vita vitendo vya hujuma,rushwa naufisadi wa kutisha katika Taifa letu.

Mwakiteleko alikuwa kioo hasa cha jamii katika kutekelezamajukumu yake,alikuwa mpole,mkalimu na mcheshi wakati wote lakini alikuwamakini zaidi katika usimamizi na utendaji wake wa kazi ambao ulimjengea heshimana nidhamu kubwa katika uongozi wake kamaMhariri kila alipokuwepo.

Tunatambua kuwa kifo ndiyo njia pekee ya kumtenganisha binadamuyoyote na ndugu zake,marafiki na jamaa wa karibu waliozoeana na kwa kuwa hayondio mapenzi ya MUNGU,tumuache Mungu aitwe Mungu na jina  lake lihimidiwe Milele…AMEN.
IMETOLEWA NA 
CHRISTOPHER NYENYEMBE
MWENYEKITI
MBEYA PRESS CLUB

(Not translated)

In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register