Base (Swahili) | English |
---|---|
Shirika la Kijogoo Group For Community Development linatafuta wadau wa kusaidiana nao katika harakati za kupinga ukatili wa Kijinsia unaoendelea Wilayani Gairo kwenye Kata za Nongwe,Mandege<Chagongwe na Chanjale dhidi ya ukeketaji wa watoto wadogo wanaosoma darasa la kwanaza na pili hasa katika kipindi hiki cha likizo. Utafiti uliofanywa na shirika letu kwa kushirikiana na Viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi ya Vijiji na Kata wakazi waishio kwenye kata hizo bado wamekuwa wakiendeleza mila zilizopitwa na wakati na tohara hasa kwa wanawake na wamebadili tabia sasa wana wakeketa wakiwa wadogo wanaosoma darasa la kwanza na la pili. Hali imekuwa ikidhalilisha utu wa mtoto na kumkosea haki zake za msingi hivyo tunawaomba wadau mtakaoguswa na ujumbe huu mtusapoti kifedha ili twende tukaweke kambi ya kutokomeza hali hiyo kwa kuendesha elimu kwa njia ya makongamano na sanaa shirikishi jamii. Ni mategemeo yetu wadau,mashirika ya ndani na nje,wafadhili wa ndani na nje na serikali pia mtatuunga mkono kwa hili lililopo kwenye jamii ya watu wa Wilaya ya Gairo inayoongozwa na kabila la Wakagulu Maombi haya yametolewa na Ramadhan Omary Mkurugenzi Kijogoo Group For Community Development Simu namba 0754 948 767 & 0715 947 897 Email - kijogoogcd@yahoo.com au ramadhankgcd@yahoo.com |
(Not translated) |