Injira

/CHACODE/post/106965: Kinyarwanda: WI0009E043E66FF000106965:content

« Inyuma   ·   Ahakurikira »
Base (Igiswayire) Kinyarwanda

ASASI ya CHACODE iliweza kufanya utafiti katika masuala ya kuhifadhi mazingira na mambo ya kale.Jambo hili limetokana na tabia ya mapokeo waliokuwa wakiitumia wazee katika kuridhishana na kupeana taarifa na kumbukumbu mbalimbali za matukio ya kihistoria,mila na desturi utaratibu ambao kwa sasa umeanza kufutika kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano na kumbukumbu.

Asasi imechukua jukumu la kufanya utafiti mdogo juu ya wazee wa kale walivyoweza kuwa na uwezo wa kufanya matukio ya kihistoria ambayo kwa uwezo wa kawaida ni vigumu kutafanya.Kwa mfano kutumia kisigino cha mguu kuweka mchoro kwenye mwamba wa jiwe na kuweka alama ambazo haziwezi kufutika.

Jambo hilo limetokea katika mkoa wa Morogoro Wilaya ya Morogoro vijijini katika eneo la makutano ya mto Mngazi na Mtombozi.Mkurugenzi Mtendaji wa CHACODE Thadei Hafigwa aliweza kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kushuhudia michoro hiyo inayosadikiwa kuchorwa na wazee wa Kabila la Waluguru Mkoani Morogoro Miongo kadhaa iliyopita

(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe