Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

TEYODEN na TYVA waongeza nafasi za ushirikiano

TEYODEN na Tanzania Youth Vision Association(TYVA),leo walifanya mkutano wa kuzindua ajenda ya vijana 2010,wakishirikisha asasi nyingine za vijana katika ukumbi wa Karimjee leo ambapo mada ilwasilishwa na mkurugenzi wa hakielimu,Bibi Annastazia Rugaba ambaye pia alibainsha changamoto zinazowakabili vijana kuelekea uchaguzi mkuu na katika harakati za kujikomboa kiuchumi,kisiasa na kiafya.

Kisha baada ya mawasilisho hayo,vijana walipata nafasi ya kufanya majadiliano yaliyopelekea kuwepo kwa maazimio ambayo baadaye yatapelekwa kwa makatibu wa vyama vya siasa nchini,yakipendekeza nini kifanyike kwa ajili ya vijana,mara chama chochote kitakachoingia madarakani kitapaswa kiyafanyie kazi.

Katika mojawapo ya maazimio hayo ni kuhusu kuwepo kwa ufuatiliaji wa mapendekezo hayo hata baada ya uchaguzi kwa wale waliochaguliwa.

 

 

 

 

 

 

August 14, 2010
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.