Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations
Kamati ya Utendaji TEYODEN yajipanga kutekeleza mradi wa Utetezi wa Mabinti wanaofanya kazi kwenye baa

Katika ile hali ya kuwajali wasichana wanaofanya kazi kwenye baa mbalimbali hapa jijini Dar Es Salaam,TEYODEN imeonelea ni vema ikajitahidi kuwatafutia suluhu ya maonevu wanayofanyiwa na wamiliki wa baa.

Katika kikao cha kamati ya utendaji kilichofanyika jumamosi ya tarehe 12 Juni 2010 katika ofisi za TEYODEN,kikihudhuriwa na mwakilishi kutoka Taasisi ya Maendeleo Shirikishi kwa vijana Arusha ( TAMASHA) yenye makao yake makuu katika jiji la Arusha,kaka Churchill Winston ambao ndio watakaokuwa wafadhili wa mradi huo na TEYODEN wakiwa ni wataalamu watafanya utafiti katika kata nne za manispaa ya Temeke ambazo ni Kurasini,Azimio, Keko na Mbagala katka baa zote zilizopo katika katika kata hizo ili kbaini ni changamoto zipi wanazokabiliana nazo mabinti hawa na jinsi ya kuzitatua wakiwashirikisha wamiliki wa baa hizo,wadau wa maendeleo katika manispaa ya Temeke na vijana mbalimbali.

Kabla ya kuingia katika mchakato huu kwanza yatakuwepo mafunzo ya namna ya kufanya utafiti huo.Mradi huo utakuwa ni wa mwaka mmoja.Kinachosubiriwa kwa sasa ni kibali kutoka wizara ya Sayansi naTeknolojia ambacho huenda kinatarajiwa kupatikana ndani ya mwezi huu.

TEYODEN itaendelea kushirikiana na mashirika mengine ikiwa ni katika kuimarisha mahusiano yake na asasi nyingine ndani na nje ya nchi.
June 19, 2010
« Previous Next »

Comments (1)

Abdi Yazidu (Kata ya Toangoma) said:
Mimi naomba semina kama hizi zikitokea kila tawi litowe mtu mmoja.
August 21, 2011

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.