Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

3. WANAHARAKATI WA WEMA WASHIRIKI MAONYESHO YA SERIKALI ZA MITAA

Tarehe 01 Julai 2010 Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya-WEMA, walishiriki katika maonyesho ya Serikali za Mitaa yaliyofanyika kiwilaya katika mji mdogo wa Ndanda Masasi. Kikundi cha WEMA kilishiriki maonyesho hayo kwa kuonyesha baadhi ya shughuli wanazozifanya. Walionyesha baadhi ya vitabu vinavyopatikana katika maktaba yao, pia walionyesha baadhi ya miche ya miti waliyootesha katika kitalu chao, hali kadhalika, walionyesha vyungu vya kupandia maua ambavyo ni miongoni mwa kazi wazojifunza kikundi cha akina mama wa WEMA, kinachojulikana kama; "WEMA WOMEN EMPOWERMENT GENERATION" ama kwa kifupi "WEMA Women - EG."

Katika picha wanaonekana watoto waliotembelea banda la WEMA wakati wa
maonyesho hayo ya Serikali za Mitaa, wakisoma vitabu. Aidha, wengine wanaonekana katika picha hiyo, ni baadhi ya wanakikundi cha WEMA ambao walishiriki wakati wa maonesho hayo. Aliyeinama na kugusa mtungi wa maua, ni Mchungaji Joseph Mwanga ambaye ni Mtunza Fedha wa WEMA.

12 Ukwakira, 2010
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.