Envaya
Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

MAARIFA YA WENYEJI NA TEKNOLOJIA YA WAAFRIKA INAVYOWEZA KULETA MAGEUZI YA KIUCHUMI NA MAENDELEO.

Bidhaa pekee katika soko huria iliyo na ushindani wa kweli ni ile inayotokana na ubunifu. Wenyeji wa Afrika wanaweza kupambana na umaskini wao wenyewe bila kutegemea misaada toka nje ya bara hili. Bara la Afrika lina malighafi nyingi, elimu, ujuzi, sayansi na teknolojia ambazo zikitumiwa kwa ufanisi, zinaweza kabisa kuleta mageuzi ya kiuchumi, kiafya na kibiashara.

Ras Mongo wa Jijini Mbeya ambaye ni mjuzi na mwenye elimu kubwa katika teknolojia na sayansi za asili ya Afrika, anathibitisha kuwa waafrika wanaweza kujikomboa kutokana na ubunifu.Ras Mongo anatengeneza na kuuza bidhaa rafiki kwa mazingira na afya ya watumiaji. Anatengeneza viatu, mapambo, viti vya kifahari na vyombo imara vya nyumbani vitokanavyo na malighafi za asili zinazopatikana kwa urahisi barani Afrika.

Vyombo vingi vya plastiki na mabati ya aluminiamu vimekuwa vikilaumiwa na wataalamu wa afya ya jamii kuwa vinaweza kusababisha kansa na magonjwa ya ini. Kutumia vyombo vya asili vitokanavyo na miti pamoja na udongo ni salama kwa afya na ni rafiki kwa mazingira, vinadumu na pia ni rafiki wa uchumi na mfuko wako. 'Africans stop being poor' anasema Ras Mongo anayepatikana eneo la Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya au kwa kumpigia simu namba 0767 589 665. Hapa chini ni baadhi ya kazi za Ras Mongo, msomi mwenye elimu, ujuzi na teknolojia za asili ya Afrika.

 

12 Machi, 2014
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Maoni (1)

Sarah (Temeke) alisema:
Napenda san hiyo designing nawez pataj
25 Juni, 2018

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.