Log in
Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Dodoma, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Kwani Viongozi wetu Hawaoni?

Wananchi wa Kata ya Hazina iliko shule ya Msingi wanajiuliza swali mkwamba "Kwani viongozi wetu hawaoni?" wakazi hawa wamefikia hatua hiyo mara baada ya kutosikia hatua zozote zilizochukuliwa na ama viongozi wa Mkoa, Wilaya, au Tarafa kuhusiana na vyumba viwili vya madarasa vilivyojengwa katika shule hiyo kuharibika vibaya kutokana na kujengwa chini ya kiwango.

Jengo hili lililojengwa kwa fedha za MMEM II; halifaimkwa shughuli zozote kutokana na kuwa a nyufa zinazotihia kila aina ya kiumbe hai kinachothamini uhai wake.

Hapa ndipo tunapojiuliza kama kweli rasilimali za umma zinatumika ipasavyo au la; jamii nayo inapaswa kuwajibika katika kusimamia vyema rasilimali za umma badala ya kuiachia serikali ambayo kazi hizi mbovu zinapofanyika viongozi wanakuwa hawahusiki.

March 8, 2011
« Previous Next »

Comments (1)

[comment deleted]
Hatimaye tumezibaini nyufa ulizo zijadili, tunakupongeza kwa kazi nzuri katika kuhabarisha jamii. Kazi njema
March 12, 2011

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.