Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Wazazi waaswa na Tuisheni za wanavyuo.

Wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Kikuyu Manispaa ya Dodoma wameaswa kujihadhari na Tuisheni zinazoendeshwa na wanavyo kwani zina madhara makubwa kuliko faida.

Rai hiyo ilitolewa kwenye mkutano wa wazazi wa wanafunzi wa kidato cha pili na cha nne wanaosoma katoka shule hiyo kufuatia malalamiko kuwa wengi wa wanafunzi wa shule hiyo wanajihusisha na masuala ya ngono na wanachuo wa St. Johns.

Wazazi na walimu wa shule ya sekondari ya Kikuyu walieleza masikitiko yao mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya maendeleo ya Kata ya Kikuyu Kaskazini Mh. Meja Risasi kuwa, baadhi ya wanafunzi wa kike katika shule hiyo wamekuwa wakisingizia kufundishwa na wanachuo hao lakini matokeo yake wanaishia kufanya nao ngono badala ya masomo.

Wazazi hao wameombwa kuhakikisha kuwa wanawalinda watoto wao dhidi ya mtego wa wanachuo kwa kuhakikisha kuwa wanawazuia kwenda kwenye tuisheni hizo bandia.

Ili kupunguza tatizo hilo; Mkuu wa shule ya Kikuyu Sekondari Bi. Mkoyi aliwaeleza wazai kuwa shule hiyo imeazimia kuwa wanafunzi wa kidato cha pili na tatu watafanya marudio ya masomo kila siku za masomo bila malipo hivyo wazazi wahakikishe kuwa wanawawezesha watoto wao angalau kwa fedha ya kujinunulia soda mchana ili wasirudi nyumbani mara baada ya masomo ya kawaida.

Wazazi waliupongeza walimu na uongozi wa shule hiyo ambayo katika matokeo ya kidato cha nne 2010 zaidi ya wanafuzi 40 walifaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu.

27 Gashyantare, 2011
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.