Envaya
Maeneo ya ukurasa huu yametafsiriwa toka (unknown language) kwa Kiswahili. Ona asili · Hariri tafsiri

Wenye Ulemavu Waomba Msaada wa Vifaa.

Watu wenye changamoto za ulemavu wamewaomba wanasiasa kuwasaidia kupata nyenzo mbalimbali kwa ajili ya shughuli zao za kila siku.

Wakiongea  kwa nyakati tofauti na MED wanachama wa Chama Cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) tawi la Dodoma wamesema; wanasiasa wana nafasi nzuri ya kutetea haki za walemavu kama kweli wakidhamiria kufanya hivyo.

Mwenyekiti wa CHAVITA tawi la Kondoa Bw. Mustafa Shabani amesema watu wenye ulemavu wana changamoto ningi za kimaendeleo zinazo sababishwa na ulemavu wao. Alisema kwamba wao kama watu wengne wanahitaji kupata taarifalakini hawazipati kwa usahihi kutokana na wao kukosa vifaa maalum vya kuongeza usikivu au wakalimani.

Naye Bw. Ally Jumanne ambaye ni katibu wa chama hicho alisema ni vema wanasiasa wakasaida kuishawishi serikali ijali haki na mahitaji ya wenye changamoto za ulemavu ili nao wanufaike na rasilimali za taifa kama wananchi wengine wasio na ulemavu.

Wadau hao wamesema kuwa vifaa vya kusaidia wenye ulemavu kama vile vifaa vya kusaidia kuongeza usikivu, kuona, fimbo maalum za wasioona na baiskeli za miguu mitatu pamoja na vifaa vingini ni ghali kiasi kwamba mtu mwenye ulemavu si rahisi kuvipata.

Walishauri serikali iwasaidie kupata wakalimani kwa ajili ya kutafsiri habari na matukio mbalimbali kupitia Televisheni na kuwasaidia wasioona kupata CD na tepu za sauti ambazo zitawasaidia kuwafikishia habari na taarifa mbalimbali kwa wakati.

26 Februari, 2011
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.