SHULE TUNAZO; VITENDEAKAZI JE?
Wakati serikali yetu ikijinadi kuwa imepata mafanikio makubwa katika kuwezesha watoto wengi kujiunga na elimu ya msingi hapa nchini; bado kuna umuhimu mkubwa wa serikali kutafakari kwa kina kile watoto hawa wanachokipata katika shuleni hizo.
Ni ukweli usiopingika kwamba shule zetu za msingi zimepata wanafunzi wengi ambao kwa hakika wamejiunga na shule za msingi kwa ajili ya kupata elimu hii muhimu kwa maisha yao ya kila siku. Kwa hili tunapaswa kuipongeza serikali kwani wapo vijana wengi ambao kwa juhudi za serikali hasa kuiptia mpango wa MMEM wangeikosa fursa hii.
Pamoja na pongezi hizi; yapo mambo ambayo tunapaswa kuyatazama kwa mapana zaidi hasa katika suala zima la upatikanaji wa vitendea kazi kama vitabu vya kiada na ziada, walimu wa kutosha kwa masomo yote, madawati, vyumba vya madarasa, matundiu ya vyoo, mazingira safi nya kujifunzia na kufundishia na viwanja vya michezo kwa watoto wetu.
Ukosefu wa mahitaji muhimu au vitendea kazi hivyo na kutokuwepo kwa juhudi za dhati za kutatua tatizo hilo ni sawa na kuididimiza elimu na kuwapotezea muda vijana hawa ambao kila kukicha wanaitafuta elimu na kujikuta ndoto zao zikiishia hewani.
Kwa kitabu kama hiki anachokisoma kijana huyu aliyefahamika kwa jina moja la Issa mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Pahi Wilayani Kondoa; ni ushahidi tosha kuwa bado kijana huyu na wengine wengi wana safari ndefu ya kutimiza ndoto zao za kupata Elimu bora na yenye manufaa kwa maisha ya baadaye.
Wadau wote wa Elimu nchini; hatuna budi kumpongeza kijana huyu kwani licha ya kitabu hiki kubaki kipande baada ya kuliwa na wadudu ambao haijafahamika kama ni jamii ya mchwa au panya; bado ameendelea kuhitaji japo masalio ya kile kilichoandikwa kwenye kitabu hiki. Hongera sana Issa!
Maoni (2)