Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

 

MIAKA SABA SHULE HAINA MWALIMU WA HESABU

Wakati serikali ikiwa imeunda tume ya kuchunguza chanzo cha matokeo mabaya ya kidato cha nne kwa mwaka 2012, zipo sababu nyingi zinazoonyesha dalili za awali za majibu yatakayoletwa na tume hiyo mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi wake.

Hivi karibuni yalitangazwa matokeo ya watahiniwa wa kidato cha nne kwa mwaka wa masomo wa 2012 na kuonyesha ya kuwa 60.1% ya wanafunzi waliofanyamtihani huo walishindwa kufikia vigezo vya kuendelea na masomo. Hali hiyo ilionekama kama kuishitua jamii na wadau wa Elimu nchini.

Pamoja na kuwa na walimu wengi waliopo vyuoni na hata wale walipangiwa vituo vya kazi shule ya sekondari ya Buigiri iliyopo katika Wilaya ya Chamwino haijawahi kupangiwa mwalimu wa hesabu kwa mika saba sasa. Hali hii imesababisha kuwepo na mwenendo wa kusuasua katika somo hilo, kwani imelazimika kwa shule kuajili walimu wa muda wa kuweza kutoa msaada wa Huduma hiyo kwa wanafunzi wake.

Akiongea na Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) katika ofisi yake Makamu Mkuu wa shule ya Buigiri sekondari Mwl. Razalo Njamasi alisema ya kuwa tatizo la kutokuwa na mwalimu wa hesabu katika shule yake ni la muda mrefu ambalo  mpaka sasa hawajapangiwa mwalimu wa hesabu katika shule hiyo, ‘Tunalazimika kutafuta mwalimu wa muda kwa ajili ya kusaidia watoto wetu lakini serikali kama serikali haijawahi kutupangia mwalimu wa hesabu na tuna mwaka wa saba sasa tangu shule hii imeanza kufundisha’, alisema mwalimu Njamasi.

Aidha tatizo la kutokuwa na mwalimu wa somo hilo linalounganisha masomo ya sayansi limeonekana kama kuwa ni janga kwa wilaya ya Chamwino limeikumba pia Shule ya sekondari ya Chamwino ambayo yenyewe ina mwalimu mmoja tu wa hesabu ambaye hutoa huduma hiyo kwa zaidiya wanafunzi 472, hayo yalibainishwa na Mkuu wa shule hiyo Bwana Fedinand Komba alipokuwa akitoa taarifa fupi juu ya maendeleo ya Mradi wa Haki zangu Sauti yangu mradi unaoendeshwa na Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma kwa ufadhili wa shirika la kimataifa la Oxfam GB ya Uingereza tawi la Tanzania.

Bwana Komba alibainisha kuwa kwa kawaida mwalimu hupaswa kuwa na vipindi 40 kwa muhula lakini kutokana na tatizo la uhaba wa walimu analazimika kuwa na vipindi visivyopungua 60 kwa muhula, kitu ambacho kinamfanya hata yeye mwalimu mwenyewe kushindwa kuwamudu wanafunzi wote kwa wakati,’badala ya kufundisha vipindi 40 mwalimu huyu analazimika kufundisha vipindi zaidi ya 60 kwa muhula kitu ambacho inakuwa si rahisi kwa mwalimu huyu kuwamudu wanafunzi kwa wakati’, alisema mwl. Komba.

Lakini pia pamoja na hayo yote katika shule nyingi kumeonekana kuna changamoto ya kutokuwa na walimu wa masomo ya sayansi kama vile katika masomo ya Chemistry na Physics kitu ambacho kwa mujibu wa baadhi ya walimu walidai inasababishwa na kutokuwa na vifaa vya kufundishia kwa vitendo katika maabara za shule.’walimu wengi wanashindwa kuja kwanza unakuta vifaa vya kufundishia hakuna na kama unavyojua masomo haya mwanafunzi anapaswa kujifunza kwa vitendo zaidi kuliko kusiliza na kuandika tu’, alisema mmoja wa walimu wa Sekondari ya Chamwino.

Kuna haja kwa serikali kukaa na kujipanga upya katika kuhakikisha ya kuwa mgawanyo wa walimu unazingatia na uhitaji wa masomo yanayokuwa hayana kabisa walimu tena kwa kuyapa kipaumbele masomo ya sayansi ambayo mara nyingi ndio huonekana wanafunzi wengi hawafanyi vizuri katika mitihani yao ya mwisho kwenye masomo haya.

16 Werurwe, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.