Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

 

Asema hata akifaulu shule ya Kata hasomi:

Mwanafunzi wa shule ya msingi Mvumi Makulu Elia Mkwila (13) amesema hayuko tayari kusoma katika shule za serikali za kata kutokana na elimu inayotolewa katika shule hizo kuto kukidhi mamhitaji ya elimu bora nchini. Kijana Mkwila ayasema hayo alipofanya mahojiano mafupi na Mrartibu wa shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) Bw. Davis Makundi wakati wa kukabidhi vitabu kwenye shule hiyo iliyoko katika Tarafa ya Mvumi.

 Hali inaonyesha wazi kuwa kwa sasa hata wanafunzi wenyewe wanaona kuwa hawata kuwa tayari kuona juhudi zao zikiishia katika shule zinazokosa vigezo vya kutoa msaada wa kuwafanya waendelee kuwa bora katika elimu yao. Kutokuwa kuwa kwao tayari kusoma katika shule za kata ni sawa na mtu anaye amua kujitoa mhanga maisha yake kama njia mojawapo ya kuonyesha kutorizika na jambo fulani.

Mwanafunzi huyo mlieleza kuwa katika masomo yake ya darasa la saba amekuwa akifanya vizuri kwenye masomo mengi ila kazi kubwa iko kwenye masomo mawili ya Hisabati na Kiingereza ambayo hufanya vibaya kila mwaka.

 Katika hatua nyinhgine mmoja wa walimu wa shule ya msingi Mvumi Makulu anakosoma kijana nElia ambaye hakutaka jina lake litajwe alieleza kuwa licha ya juhudi kubwa za walimu katika kufundisha, bado ana mashaka makubwa na hai itakavyokuwa kwa wanafunzi wa darasa la saba wakati wa mtihani. “watoto hawa wanahitaji kazi ya ziada katika kuwasaidia katika mtihani wao wa darasa la saba kutokana na masharti ya kutumia karatasi za (OMR)”.

25 Gashyantare, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.