Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

WATAKA WABUNGE WAJITOKEZE KWENYE MIDAHALO.

Wananchi wa majimbo ya uchaguzi ya Mtera na Chilonwa katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma wamewataka Wabunge wao kujitokeza katika mijadala inayowakutanisha ili wapate fursa ya kujadili juu ya matatizo yao. Wapiga kura hao waliyasema hayo katika mahojiano ya ufanisi wa mijadala ya Mahusiano baina ya Wabunge na wananchi inaypfadhiliwa na shirika la The Foundation for Civil Society na kuratibiwa na Asasi ya CHANGONET ya Wilaya ya Chamwino.

Wananchi hao wameeleza kuwa wanakabiliwa na kero mbalimbali ambazo Wabunge wao walipaswa kuzijadili pamoja na kuzipaia ufumbuzi lakini hawajitokezi kuwasikiliza na kuwasababishia usumbufu mkubwa. "hapa kijijini tunakabiliwa na matumizi mabaya ya ardhi na wakati mwingine wanakuja watu wanajifanya wawekezaji na kutudhulumu ardhi yetu, watetezi wetu hao wabunge hawaonekani" alisema Bibi. Kurwa Mkazi wa kijiji cha Manchali.

Wananchi hao walihoji sababu za baadhi ya viongozi wa kisiasa kushindwa kujitokeza katika mikusanyiko ya wananchi wakati wao ndio wahamasishaji wa maendeleo katika maeneo yao na kuwasimamia watendaji wa serikali. 

Walimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Bi. Fatma Said Ally kutokana na juhudi anazozionesha kila wakati katika Wialya hiyo na kushauri viongozi wa kisiasa kuiga mfano wa kiongozi huyo. "Mkuu wa Wilaya ameteuliwa na Rais lakini anaonyesha kutujali na kushiriki kwenye mijadala; hao tuliowapigia kura wanajifanya wana kazi nyingi kila tukiwahitaji, kama hizo nafasi zina kazi nyingi waziache wapewe wengine"

Mijadala ya kuimarisha mahusiano na Wabunge katika Wilaya ya Chamwino imekuwa ikifanyika na kukosa ushirikiano wa karibu kutoka kwa Wabunge licha ya uongozi wa Wilaya na Halmashauri kutoa ushirikiano katika kufanikisha Mijadala hiyo.

Tangu mijadala hiyo ianze mwaka 2012 imekuwa ikihudhuriwa na viongozi wa ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ila Wabunge na Madiwani wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kutosha.

15 Gashyantare, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.