Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Icyongereza. Edit translations

small.jpg

Shule ya Sekondari nanyamba iliyopo kata ya nanyamba wilaya ya Mtwara vijijini

small.jpg

Kijiji cha nanyamba kilicho karibu na kata ya nanyamba Halmashauri ya Mtwara Vijijini

small.jpg

Maeneo ya shule zilizopo mkoani Mtwara

Mpango wa utoaji wa elimu ya watu wazima vijijini uungwe mkono

Na ASIA KILAMBWANDA

Taaluma ni nyenzo kubwa ya kufikia maendeleo , pia huharakisha mipango ya kufika katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na hata kisiasa bila kujali taaluma hiyo ni nadharia ama vitendo inategemea jinsi ya matumizi ya taaluma hiyo.

Katika kulifahamu hili Halmashauri ya wilaya ya Mtwara Vijijini kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la kuwahudumia watoto (Unicef), imeandaa mpango wa utoaji wa elimu kwa watoto waliopita muda wa kuandikishwa kujiunga na elimu ya shule ya msingi, elimu ya watu wazima ujulikanao kama MENKWA .

Mpango huo umetoa mafunzo ya walimu watakaoshiriki kakika ufundishaji wa wanafunzi watakaosoma elimu ya watu wazima(MENKWA),katika mkakati wa kuondoa ujinga na umasikini na kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma na kuandika .

Mafunzo haya yaliwashirikisha 60 na wadau wa elimu katika ngazi ya kata ili kukidhi mahitaji ya wananchi na watoto katika utoaji wa elimu husika bila kuathiri kundi au nafasi na haki ya kupata elimu.

Baadhi ya kata zilizoshiriki ni Naumbu, madimba, Tangazo, nanyamba, likomnde, Dihimba, Msimbati, Nitekela, Mgau na Malanje. Na nyingine ni mayembe chini, mchanja, msanga mkuu, chawi, libobe, Bandari, kilambo na Nachenjele.

Matarajio ya elimu au taaluma yeyote katika jamii ni kuona kwamba inaleta tija na mabadiliko katika nchi, kwa mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

Kwa hali hii mpango wa kutokomeza ujinga hasa katika maeneo yaliyosahaulika(Vijijini) utaondoa ufinyu wa kufikiri unaowafanya vijana wengi washindwe kujituma kutokana na ukosefu wa elimu jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya vijana.

There has been a setback in the reception of the broadcasting of the JEAN media's only communty radio existing in the Southern Mtwara region,when our antenna was pulled off the tower owned by our kind neighbours The Artmus Electricity company, who had to vacate original premises due to a sudden termination of their contract.

Meanwhile JEAN media intends to purchase from Miami Florida OMB,USA, a Mr PLATINUM LINK receiver for frequencies 175 MHz TO 470 MHz supplied in 20 MHz bands ,at the rate of $1,700.00. The equipment is extremely synthesized, LCD screen display for parameter selection and readings as frequency (6digits), RF level sub-carriers level,with mono stereo (MPX), AND 3 SCA audio outputs and remote control. This multi purpose device is expected to settle the attena problem, ensuring excellent reception of our broadcasts.

Currently , providing Irf cable to Radio Maria in Mtwara, Clouds FM radio in Mtwara having somewhat similar setbacks, in collaboration with Mtwara Communty radio, will diplex in their shelter and then radio Maria will diplex the signal of the two radio stations with Radio Maria, shelter.

In this case,clouds FM radio and Mtwara communty Radio will diplex between them with a stereo type combiner and then provide the output to radio maria.

with this setup Mtwara communty Radio will effectively be on air as JEAN media solicits funds for the radio link receiver mentioned earlier. 

Umoja_wa_wamiliki.pdf

Executive chairperson of Jean media, Mrs Sango Kipozi has been selected to be Executive chair for the commitee of the Southern Radio station owners the documents above specify her position and the role of the members of the commitee

JEAN MEDIA, KUPITIA MTWARA FM,REDIO YA JAMII, IMEFUATILIA ATHARI YA MAZINGIRA KUTOKANA NA MABOMU YALIYOLIPUKA KATIKA KAMBI  YA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA KIKOSI NAMBA 511 KATIKA ENEO LA GONGO LA MBOTO JIJINI DAR-ES-SALAAM 

Milipuko mikubwa ya mabomu iliyotokea inchini Tanzania katika ghala kuu la kutunzia silaha la jeshi la wananchi wa Tanzania [JWTZ] Gongo la mboto jijini Dar es salaam imesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.

Milipuko hiyo iliyotokea tarehe 16/02/2011 majira ya saa mbili usiku imesababisha taharuki kubwa na hofu  miongoni mwa wakazi wa jiji la dar es salaam na pia kusababisha watu na wanyama kukimbia huku na huko kujinusuru maisha yao.

Hali kadhalika milipuko hiyo mikubwa imesababisha uharibifu wa mazingira, ikiwa ni pamoja na kupoteza uoto wake wa asili yake, kufuatia moto uliounguza majani. Mabomu yalikata miti na baadhi ya maeneo kutifuliwa, na pia nyumba kuteketea kwa moto.

Uchafuzi wa  mazingira uliosanabishwa na milipuko hiyo, umeathiri mno hali ya hewa na kuichafua kwa kuifanya  kuwa nzito,  kutokana na kuchanganyika na moshi mkali. Vilevile wananchi wanahisi kuwa hewa wanayovuta imechanganyika na sumu,  kwa kile walichokisema kuwa asilimia kubwa ya wahanga miongoni mwao, wanakohoa kwa kipindi kirefu, tangu kutokeee kwa tukio hilo.

Watu ishirini na mbili [22] wamepoteza maisha yao   na wapatao mai tatu[300]kujeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao ,na wengine kupata vilema vya kudumu, kama vile kukosa mikono au miguu, na pia kupoteza sehemu nyingine za miili yao.

Viumbe vingine ni pamoja na wanyama, wadudu na ndege waliopoteza uhai wao katika milipuko hiyo.

kwa mawazo yangu, nadhani kuwa kwa athari zilizo jitokeza katika milipuko hiyo, hapana budi kwa nchi ya Tanzania kutafuta ufumbizi wa haraka, ili kunusuru uharibifu mkubwa wa mazingira utakaoendelea kujitokeza kama mmomonyoko wa udongo, ukosefu wa hewa safi na uchafuzi wa mazingira, ili kulinda afya za jamii na kuboresha maeneo ambayo kabla ya milipuko, yaliyokuwa yakitumika kwa kilimo cha mboga mboga.

NA LEONIA LUCAS MAHONA

 

     Jean media imetoa msaada wa katoni za maji , na vitafunio mbalil mbali vya watoto kwa wahanga wa janga la kitaifa lililo tokea Gongo la Mboto juzi ambapo mabomu yali lipuka ghafla kwenye ghala za mabomu ziliopo eneo la Gongo la mboto. mpaka sasa watu 20 wamekwisha poteza maisha yao na 300 ni majeruhi. Janga hili limewahi kutokea hapo Mbagala.