Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI WILAYA YA  MULEBA- KAGERA

 

Shirika la Kwa wazee Nshamba Muleba kwa kushirikiana na Wazee ,walengwa liliadhimisha siku ya Wazee Duniani yaani tarehe 1 OTOBA 2012.

 Siku hiyo ilikuwa ya vifijo shangwe na nderemo kwa wazee wa kata saba za wilaya ya MULEBA na wanajamii waishio maeneo ya kata Nshamba, wajukuu wanao tunzwa na Wazee na wafanyakazi wa shirika, pamoja na wageni walioalikwa .

 Ikiwa ni mwaka wa nne kuadhimisha sherehe hizi , sherehe hiyo ilihudhuriwa na wazee wapatao 650 robo tatu yao wakiwa ni Wazee wanaopata pensheni toka shirika la Kwa Wazee.

 Michezo mbali mbali pamoja na nyimbo na risala vilivyoandaliwa na Wazee vilibeba ujumbe unaohusu maisha ya Wazee na changamoto wanozokumbana nazo, kama vile kutopatiwa matibabu bure,  mzigo wa kulea na kutunza wajukuu, umaskini kwa wazee,na ukatili wanaofanyiwa Wazee lakini pia   kuiomba serikali kutoa pensheni kwa wazee wote ili kuboresha maisha yao kama ambavyo nchi nyingine   zimeweza kufanya.

 Akijibu risala hiyo, aliyekuwa mgeni rasmi katika madhimisho hayo Mhe Nashon Kababaye katibu tawala wilaya kwa niaba ya mkuu wa wilaya,

Aliwapongeza wazee kwa kuona umuhimu wa kuadhimisha sherehe hiyo pia aliupongeza uongozi wa Kwa wazee kwa jitihada zao za kuboresha maisha ya wazee hapa wilayani Muleba.

 Mgeni rasmi alikemea   vitendo vya ukatili kwa wazee na kuwataka waganga wote   wanaopiga ramli   kujisajiri kabla ya mwaka 2013 vinginevyo watakamatwa maana ndio wanaochangia vitendo hivyo.

 Pia mgeni rasmi alisisitiza na kutoa rai kwa wazee kuwa ni haki kwao kupatiwa matibabu bila malipo hivyo iwapo kutajitokeza utata alitoa namba za simu ili taarifa zitolewe  ili uongozi uhusike kuwapatia  ufumbuzi. Kuhusu pesheni kwa wazee wote   alisema ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa upo uwezekano wa kulipa pensheni kwa wazee walio na umri wa miaka 60 na kuendelea.

 Aliomba ushirikiano na uwazi kwa matukio ya ukatili pindi yanapojitokeza ili kusaidia  

ufuatiliaji na kuwawajibisha wahusika. Aliwaomba wao pia, wawe na uchungu kwa maisha yao na mali zao.

 Naye kaimu mratibu wa shirika la kwa wazee , Ndg Edmund Revelian aliwapongeza na kuwashukuru wazee na wageni wote kwa mwitikio wao , katika maadhimisho hayo muhimu. Aliwaomba wanajamii na serikali kuuthamini uzee, kwani uzee si hiari bali ni hatua ambayo kila mmoja ataipitia.

 

 

2 Ugushyingo, 2012
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.