Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Zantel na TEYODEN wafanya programu ya ushirikiano ili kuwezesha vijana kuongeza kipato chao na kuwa na uwezo kukabiliana na changamoto za kimaisha.

Vijana wa kata ya kilakala wamefanya kikao cha pamoja na katibu mtendaji wa TEYODEN na mhamasishaji jamii wa kampuni ya ZANTEL.Lengo la kikao ni kufanya majadiliano ya pamoja na kukubaliana juu ya ushirikiano wa pamoja kati ya pende hizo mbili.mhamasishaji wa ZANTEL alieleza kuwa vijana wanaweza kujiunga na kampuni hiyo ya simu na kupata faida ya asilimia zaidi 10 kwa uuzaji wa bidhaa za kampuni hiyo wakati pia wakiongeza pato lao kama kikundi.Akiongeza maelezo ya mhamasishaji bwana Katibu mtendaji wa TEYODEN bwana Yusuph Kutegwa aliwataka vijana wa Kilakala kuwa mfano kwa kulichukulia maanani suala hili la kijasiriamali ili kuleta tija kwa vituo kuliko kukaa na kuwezeshana kielimu pekee.Zoezi hili la Vikao na vijana litaendelea katika kata za Azimio,Mtoni,Mbagala,Toangoma,Kibada,Vijibweni na pemba mnazi.

November 8, 2011
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.