Envaya
Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

Mafunzo ya project management Naivasha Kenya yatakuwa chachu ya mabadiliko ya vijana kuelekea ujasiriamali na utengenezaji ajira binafsi kwa vijana.

Siku 8 za mafunzo ya uendeshaji wa miradi yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na ILO  y2y fund pamoja na UNHABITAT youth fund zimebadilisha mtazamo wa mameneja 10 kutoka Tanzania.Mameneja hao kwa sasa, wanafikiria kuboresha miradi 10  ambayo ILO wameichagua kati ya miradi 103 iliyoombwa katika mfuko huo wa vijana kwa mwaka 2012.miradi ya mwaka huu imegusia maeneo ya taka ni pato,ulimaji wa mboga mboga kwa njia za kiasili,uongezaji wa thamani katika mazao ya chikichi,uvunaji wa asali,uboreshaji wa sabuni za maji na utengezaji wa batiki,uboreshaji wa bidhaa za ngozi,new chips vending,uboreshaji wa mazao ya muhogo kutengeneza biskuti.

Mameneja watakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa miradi inakwenda vizuri na kutoa ajira kwa vijana nchini Tanzania.

Mafunzo yalikusanya mameneja wa miradi kutoka nchi za Togo.benin,zambia,kenya uganda,malawi.kongo,Tanzania,mauritius,misri na nyingine nyingi.

Hata hivyo mifuko hiyo itaendeleo kuwezesha vijana barani afrika na kwingineko kuwawezesha vijana kuongeza ajira binafsi kwa kuwa tatizo la ajira rasmi na zenye tija limekuwa ni kubwa sana.


27 Februari, 2013
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Maoni (3)

R.J. Chatta (Kisarawe District) alisema:
Nawapongeza sana kwa juhudi zenu za kuwafanya vijana kujitambua na kuwa chachu ya maendeleo. Maranye agro processing social business ipo tayari kufanya kazi nanyi katika sector ya ukulima wa mboga mboga katika masha yetu ya mboga huko kisarawe
2 Machi, 2013
suleiman Jeni (MWANAKWEREKWE-ZANZIBAR) alisema:
Hongereni sana mtandao wa vijana wa Temeke. Napenda kuchukua fursa hii kwa kuuomba uwongozi wa TEYODEN kushirikiana na sisi vijana wa Asasi ya MEECO ili tubadilishane uzoefu kwa lengo la kuboresha shughuli zetu zaidi pamoja na kuunda udugu na mshikamano
5 Aprili, 2013
Shani Kutegwa (Dar-es-salaam) alisema:
Nawapongeza sana TEYODEN kwa kweli ni mtandao unaolenga kuborsha maisha ya vijana Tanzania big up.
10 Aprili, 2013

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.