Hali hii ya watoto kula majalalani itaisha lini? tushirikiane kuokoa kizazi hiki ambacho ni tegemeo la Taifa.
Wanafunzi wa darasa la pili wa shule ya Msingi Yala wilayani Mbarali mkoani Mbeya wakiwa nje ya madarasa yao wakijifunza kuhesabu kama walivyokutwa na Ezekiel Kamanga wa Shirika lisilokuwa na Kiserikali la TANZANIA COMMUNITY MEDIA ORGANIZATION (TACOMO)
Kulia ni Mtunza hazina wa TACOMO Ezekiel Kamanga akiwa na Mkurugenzi wa TACOMO wakitafakari jambo.
Je uvunaji huu wa kisasa unaoendelea katika shamba la shirika la kilimo Uyole Jijini Mbeya, wakulima wadogohasa vijijini watafikia hapo?
Wakina Mama wajasiliamali katika Kata ya Mshangano Manispaa ya Songea wakiuza mazao ya mbogamboga chini katika Soko la Mshangano ambapo wamekuwa wakitozwa ushuru wa kati ya Shilingi 200 na 500 kwa siku kutokana na biashara hiyo,licha ya kuwa ni hatari kwa afya za watumiaji,imekuwa ikishangaza kuona Manispaa inachukua ushuru bila kujali kutengeneza miundombinu stahiki katika soko hilo jambo ambalo linatafsirika kama ni kuwadhulumu wakina mama hao miaka 50 ya uhuru.
Daraja la udongo hilo je ni salama ama ni kushindwa kuwajibika kwa viongozi tunaowachagua?!!!