Kwani Viongozi wetu Hawaoni?
Wananchi wa Kata ya Hazina iliko shule ya Msingi wanajiuliza swali mkwamba "Kwani viongozi wetu hawaoni?" wakazi hawa wamefikia hatua hiyo mara baada ya kutosikia hatua zozote zilizochukuliwa na ama viongozi wa Mkoa, Wilaya, au Tarafa kuhusiana na vyumba viwili vya madarasa vilivyojengwa katika shule hiyo kuharibika vibaya kutokana na kujengwa chini ya kiwango.
Jengo hili lililojengwa kwa fedha za MMEM II; halifaimkwa shughuli zozote kutokana na kuwa a nyufa zinazotihia kila aina ya kiumbe hai kinachothamini uhai wake.
Hapa ndipo tunapojiuliza kama kweli rasilimali za umma zinatumika ipasavyo au la; jamii nayo inapaswa kuwajibika katika kusimamia vyema rasilimali za umma badala ya kuiachia serikali ambayo kazi hizi mbovu zinapofanyika viongozi wanakuwa hawahusiki.
Ibitekerezo (1)