Envaya

Furaha ya Wanawake Wajasiriamali  kwa Viziwi Tanzania (FUWAVITA)  ni Asasi iliyosajiriwa na kutambulika Kisheria kwa Namba 17120 na inawajumbe 17. Asasi hii ilianzishwa kutokanana na  Utafiti uliofanywa na Bi Aneth Gerana  ambapo aliwezeshwa na Shirika la Maendeleo ya Walemavu (ADD) Kutafiti katika Asasi mbalimbali zinazowahusu Viziwi , na kugundua kuwa Asilimia 49ya Wanawake Viziwi wamepatwa na Matukio ya Uzalilishwaji  na Unyanyasaji wa kijinsia ikiwa ni pamoja  nakukabiliwa na hali Ngumu ya Maisha kwani wengi wao wanafamilia ambazo zinawategemea hivyo  ndio hukawa Mwanzo wa kuzaliwa kwa  Chombo hiki cha kuwakomboa Wanawake Viziwi  ili kutetea haki zao kupitia Ujasiriamali.

Asasi ilianza shughuli zake mwaka 2008 lakini rasmi mwaka 2010 ilipopata usajili kamili Waanzilishi ni  Kiziwi aliyehitimu Chuo Kikuu cha Dar es slaama ambaye ni wa kwanza kuweza kufika chuo kikuu Tanzania kwa kushirikiana na Wanzake waliomaliza katika Vyuo  binafsi vya Ualimu ambao hawakufanikiwa kupata Ajira kutokana na Ukiziwi wao. Tanzania Bara kuna asasi nyingi za kiraia ambazo zimekuwa zinatetea wanawake Nchini lakini hakuna hata moja iliyosimama imara kusimamia na kutetea mwanamke Kiziwi