Envaya

Africa Upendo Group

Dar es Salaam Flooding Community Survey

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Dar es Salaam Flooding Community Survey

Mtaa wa mwongozo Lukas Sekelo
barabara,maji,miundo mbinu,fedha na makazi
nyumba yangu nusu imezolewa na maji
maisha ni ya shida sana kwani tunaishi juu ya mto hakun tena nafasi sehemu kubwa imechukuliwa na maji
maji hayafai kabisa
Before flooding: (No Response)Now: (No Response)
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (1)

Africa Upendo Group (Makuburi - Kinondoni Dar es salaam) bavuzeko

Katika kata ya Makuburi Wilaya ya kinondoni mafuriko yaliharibu nyumba za wakazi zaidi ya 261.Kusema ukweli hali ilikuwa mbaya sana.Tulishuhudia watu wengi wakibebwa na maji hasa mateja ambao wengi walikuwa wanaishi mitoni wakivuta madawa ya kulevya pia walikuwa wakijaribu kuokoa au kuchukua mali mbalimbali zilizokuwa zikibebwa na maji.Maji yaliingia hadi ndani ya nyumba nyingi kiasi kuwa vitu vyote vilikuwa vikielea na maji na kuharibika kabisa.Leo wakazi wengi wanaishi maisha ya taabu kwani hakuna anayewajali ni ahadi tu ambazo hazijatekelezwa hadi kesho.Watoto wengi hawaendi shule kwani bado hali ni ngumu sana kwa wazazi wengi na wengine wamehama kabisa maeneo yao kwani hakuna kitu na kutokana na ratiba ya makazi kuharibika wengi wanaishi mahali ambapo shule waliyokuwa wanasoma ziko mbali sana na wanapoishi hivi sasa.Haki ya watoto ya kusoma imekuwa ni kama hazifuatwi tena.
akina mama ambao wengi walikuwa wajasiriamali wameacha shughuli zao kwani nyingi zilibebwa na maji mfano wale walikuwa wanapika vitumbua maandazi mihogo samaki n.k hawana tena mitaji na vyombo vimezolewa na maji.
Nilikutana na Case ya shangazi yangu ambaye anaishi pale Jangwani ambaye baada ya maji kujaa na kuondoka alikimbilia kwa mwanae Mbagala.Sasa anasema anapata sana taabu kwa vile inabidi kila kitu lazima aombe.Yeye ameshakuwa mtu mzima hajiwezi tena japo ana nguvu lakini kutokana na mafuriko haya anasema hawezi tena kurudi na kuendelea na shughuli zake za kila siku.Anasema kwa nini serikali isitafute njia mbadala ndio pamoja na wao kuhama lakini bado tatizo halijatatuliwa.
Kwa nini wasiihamishe njia ya maji kama wengine wanavyofanya yaani nchi zingine wanavyoweza kubadilisha matumizi mbalimbali kwa kutumia nyenzo mbalimbali.Pia Deo naye anapendekeza kuwa serikali inatakiwa kutafuta Mbinu mbadala badala ya kuwahamisha wananchi wanatakiwa kutumia miundo mbinu ya kisasa ili kufanya maeneo hayo yaliyoathiriwa na mafuriko kutumika tena bila athari yoyote.
Maeneo mbalimbali ya Barabara yameharibika sana mfano kuna daraja liko hapa External ambalo linaunganisha barabara ya Ubungo Mandela,Ubungo Maziwa na barabara ya Kigogo ambalo ni nyezo kubwa sana ya mawasiliano na ktokana na mafuriko Daraja hilo limemeguka kiasi kuwa wakati wowote linaweza kudidimia na kuwaaacha wakazi wake wakiwa katika hali ngumu.Lakini pia kuna daraja linginelinaunganisha barabara inayotokea Tabata TIOT na kuingia Kigogo hadi Mburahati karibu na shule ya Gozage na kanisa katoliki liko katika hali mbaya sana na lina wakazi wengi sana wanalolitegemea na ni njia ya rahisi sana kuunganisha kigogo,Mabibo na Tabata lakini sasa liko katika hali mbaya sana.Pia kuna barabara ya Kisukuru ambayo inaunganisha wakazi wanaotokea Ubungo na Tabata hadi Makoka iko katika hali mbaya sana imebaharibika vibaya sana na imebakia kidogo sana kuachane na wakazi wengi watapata shida sana hasa wale wa Tabata Kimanga Kisukuru na Makoka.
Hivi sasa wakazi wengi hawapati maji huku katika eneo lote la Mabibo Makuburi na Tabata kwa sababu miundo mbinu ya kuleta maji imeharibiwa sana mabomba yamezolewa na mafuriko na wakazi wanauziwa maji kwa bei ya juu sana kuanzia Tsh 300 kwa ndoo na kuendelea.
Leo hapa katika Serikali ya mtaa wa Mwongozo waliandamana na kumwendea mwenyekiti wa serikali ya mitaa na ndoo zao kichwani walikuwa akina mama wengi sana na ndoo kila mtu zaidi ya kumi kumi wakimtaka awapatie maji.Mwenyekiti alikuwa na hali ngumu sana na ilibidi awasiliane na viongozi mbalimbali wa Dawasa na kuwaelezea hali halisi iliyopo ofisini kwake.Magari mengi sana yanapita kuuza maji na kujipatia hela kibao kwa waathirika hawa wasiokuwa na kitu na kutokana na hali zao ndio maana waliona vema kuandamana.
Pamoja na juhudi mbalimbali zilizofanywa na viongozi hawa wa kata hii ya Makuburi kwa kwenda kwenye ofisi za Dawasa zilizopo Tabata na kuahidiwa kusaidiwa lakini bado hali imeendelea kuwa ngumu na huenda ikawa magonjwa mbalimbali yakajitokeza kwani hakuna maji salama na masafi ya kutumia.

Hapa ni Ofisi ya Africa Upendo Group.Hawa ni baadhi ya Vijana ambao ni nguvu kazi ya Asasi hii wakipanga mikakati ya jinsi ya kuboresha Mipango mbalimbali waliyojiwekea hasa baada ya zoezi zima la Kutembelea wahanga wa Mafuriko.Hapa Mwenyekiti wa Asasi hii ndugu Neatness Msemo akijaribu kusisitiza jambo na vijana wakijaribu kutafakari.Aliyeketi mbele ya meza ni Kijana David.Huyu kijana kwa wale ambao wanafuatilia mambo alikuwa ni Spika wa Bunge la wanafunzi.Kulia kwake mwenyekiti ni Kijana Frank Malaki ambaye naye kwa pamoja na vijana wengine wanakuja na Kipindi ambacho kitarushwa hivi karibuni cha ' Balozi ' na Kijana Deogratius Nyusso ambaye ndiye Training Manager anayeratibu shughuli zote za Ofisi na Asasi kwa ujumla.Ukifika hapa ofisini na kuwaona vijana hawa hutasita kuwasikiliza.Karibuni sana.

 

13 Gashyantare, 2012 (edited 13 Gashyantare, 2012)

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.