Injira

/BWJMT: Kinyarwanda: WIMOBx6BIIWqZ2TSNB2vMmWD:content

« Inyuma   ·   Ahakurikira »
Base (Icyongereza) Kinyarwanda


DIRA

 

Dira ya Baraza ni kuwa chombo imara cha kutetea haki za watoto na kuhamasisha Utekelezaji wa haki hizo na kuelimisha watoto na jamii kuhusu haki na wajibu wa mtoto  ili kujenga Tanzania bora na dunia imfaayo kila mtoto. 

DHIMA

 

Dhima ya Baraza ni kuwaunganisha na kuwajenga watoto wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mazingira bora ya kidemokrasia na kupata uzoefu wa kushiriki na kushirikishwa kikamilifu katika uwakilishi katika michakato mbalimbai ya kisera na ufanyaji maamuzi ili kulinda na kutetea ipasavyo haki na maslahi ya mtoto ili kufikia azma ya kuwa na Tanzania na dunia imfaayo kila mtoto ili kuwezesha watoto kulelewa vema na kufikia upeo wa uwezo wao kiakili, kiafya, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

MALENGO

Baraza la Watoto wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litakuwa na madhumuni yafuatayo:-


Kutoa fursa kwa watoto kusikika kupitia mikutano ya kitaifa na kimataifa ya majadiliano kuhusiana na masuala yanayowahusu watoto.


Kujenga ushirikiano wa karibu kati na baina ya watoto, vyombo vya habari, mashirika yasiyo ya kiserikali na Serikali.

Kuhakikisha watoto wanapata habari na taarifa sahihi zinazowahusu.


Kufuatilia utekelezaji wa sera na sheria mbalimbali za nchi zinazowahusu watoto.


Kuelimisha jamii na watoto juu ya haki na wajibu wa mtoto.


Kushiriki kwenye harakati za watoto duniani na ufuatiliaji wa mikakati ya Azimio la ‘Dunia Iwafaayo Watoto’.


Kujenga uhusiano na ushirikiano na Mabaraza na Mabunge mbalimbali ya watoto duniani.


Kukuza na kubadilishana uzoefu na ujuzi na Mabaraza na Mabunge mengine ya watoto duniani katika kupigania haki, wajibu na maendeleo ya mtoto. 


Kutetea haki za watoto na maslahi ya watoto wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

 

(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe