Base (English) | English |
---|---|
Tumeona tuchambue wazo lenu na kulimega mafungu matano: Kujenga Uwezo wa wanachama wenu na viongozi wa Kikundi/Shirika/ Chama au Asasi yenu kwa pamoja au kwa nyakati tofauti kwa: a) Kubainisha mahitaji ya msingi (vipaumbele) b) Kuangalia udhaifu wa asasi na Uwezo wa Asasi na kujibobeza katika jambo moja au kadhaa c) Kuingia kwa undani katika dira ya Asasi (mtazamo, imani, madhumini na shughuli) d) Kuongeza kipato (fund raising) na mbinu zake e) Kujenga uhusiano, kutandaa, kushirikiana na asasi nyingine za kitaifa, kikanda na kimataifa Haya yanachambuliwa kitaalam kwa kuyaainisha katika mikakati, mipango na sera kwa kuzingatia muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Kimsingi haya yote hujengwa kwa kuzingatia falsafa inayoongoza asasi kutoka ndani na nje ya asasi. Ili kupata dhana nzima ya falsafa ya asasi pia utafiti kubainisha mapungufu ya jamii inayowazunguka hufanyika. Kwa mfano unataka kuandika mradi wa kutokomeza umaskini katika Kijiji J. Lazima kuangalia katika dira (vision), mtazamo (mission), madhumuni (objectives) ya asasi yenu kuna kipengere cha kutokomeza umaskini? Ukitaka kupanga mikakati ya asasi utafanya hivyohivyo. Utajiuliza maswali mfano hali ikoje kwa dunia, ukanda wa Afrika na Afrika Mashariki, Tanzania, mkoa wako, wilaya hadi kijiji hicho. Utafiti utakuwezesha kupta data/hadari na takwimu sahihi za kusaidia kujenga hoja kuhusu mradi wa kutokomeza umaskini katika Kijiji J. Kuna mengi ya kuangali tukichambua moja baada ya jingine na mabingwa wamefanya tafiti nyingi na kuandika vitabu na machapisho mengi. Haitoshi kuzungumzia suala hili kwa uchache wa maelezo haya. Tunalo darasa la kuandika miradi, kuwezesha vikundi vya vijana na wanawake, tumeunda pia vikundi vyetu, tunatoa mafunzo ya ujasiriamali, uongozi wa vikundi na asasi za aina zote, Tutafute tunapatikana katika website yetu: www.envaya.org/rural-media4-change au piga simu 0755893303 au baruapepe: benno.apondo@gmail.com |
(Not translated) |