Log in

/indabaafrica/post/jk-aomboleza-kifo-cha-luteni-jenerali-mst-silas-peter-manyung,48622: English: WI0007EAA944120000048622:content

« Previous   ·   Next »
Base (Swahili) English

MUSUGURI+%2528KULIA%2529+NA+SILAS+MAYUNGRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, kuomboleza kifo cha Luteni Jenerali (Mst) Silas Peter Manyunga kilichotokea alfajiri ya saa 10.30 kuamkia leo katika Hospitali ya Apollo, mjini New Delhi, India. Jenerali Manyunga amefariki akiwa na umri wa miaka 71.

“Nimepokea kwa mshtuko na huzuni habari za kifo cha Jenerali Silas Manyunga. Nilimfahamu binafsi Jenerali Manyuga katika uhai wake. Alikuwa askari hodari wa jeshi letu. Alikuwa kamanda wa kutumainiwa wa ulinzi wa nchi yetu, “amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“Katika maisha yako yote Jenerali Manyunga alidhihirisha na kuthibitisha uzalendo wake kwa nchi yake na moyo wake wa kujituma kulinda amani, usalama na utaifa wa nchi yetu na taifa letu. Jeshi letu limendokewa na mtu muhimu wa kulipa ushauri wakati ushauri wake ulikuwa bado unahitajika.

Ameongeza Mheshimiwa Rais: “Hata baada ya kutoka katika utumishi wa jeshi, Jenerali Manyunga aliendelea kuonyesha sifa hizo hizo za uzalendo na moyo wa kuitumikia nchi yake katika nafasi nyingine akiwa Katibu wa Chama wa Mkoa, akiwa Balozi wa Tanzania katika nchi za Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na hata baada ya kustaafu utumishi wa umma. Nchi yetu imempoteza mtumishi wa umma hodari na mzalendo.”

Amesema Rais Kikwete: “Nakutumia wewe Jenerali Davis Mwanyunge, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, salamu za rambirambi za dhati ya moyo wangu kufuatia kifo hicho. Kupitia kwako, nakuomba uwasilishe salamu na pole zangu nyingi kwa familia, ndugu na jamaa wa marehemu kwa kuondokewa na baba, mzazi, mlezi na mpendwa wao. Aidha, napenda kupitia kwako uwasilishe pole zangu kwa wanajeshi wote wa Tanzania kwa kupotelewa na askari mwenzao na Kamanda wao.”

Amesisitiza Mheshimiwa Rais, “ Wajulishe wana-familia ya marehemu na wanajeshi wote wa Tanzania kuwa moyo wangu uko nao katika msiba huu. Huzuni yao ni huzuni yangu. Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, awape moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Yote ni Mapenzi yake na aiweke Peponi Pema Roho ya Marehemu. Ameni.”

Luteni Jenerali Silas Peter Manyunga alizaliwa Maswa, Shinyanga mwaka 1940. Alijiunga na Jeshi la Tanganyika Rifles Januari 10, mwaka 1963, baada ya kumaliza elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari ya Bwiru, Mwanza. Alihitimu kozi ya Uofisa wa Jeshi Julai 26, 1963, nchini Israel, akahitimu kozi ya Unadhimu na Ukamanda wa Jeshi mwaka 1973 nchini Canada na kuhitimu kozi ya Ukamanda wa Juu wa Jeshi mwaka 1974 hapa nchini.

Alipandishwa cheo na kuwa Luteni Jenerali Juni 21, mwaka 1995 na kabla ya kustaafu jeshini Desemba 31, 1995, alipata kuwa Mkurugenzi wa Mafunzo katika Makao Makuu ya Jeshi, Mkurugenzi wa Tawi la Mafunzo Makao Makuu ya Jeshi, Kamanda wa Brigedi ya 202 ya Tabora, na Kamanda wa Divisheni za 20 na 30 za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Jenerali Manyuga alishiriki kikamilifu Vita Dhidi ya Iddi Amin katika Operesheni Chakaza ambako alikuwa Kamanda wa Brigedi ya 206 na baada ya hapo kuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha JWTZ nchini Uganda kati ya 1979 na 1980.

Mbali na jeshi, Jenerali Manyunga alitumikia umma kama Mkuu wa Mkoa wa Singida mwaka 1977 – 1978, Katibu wa Chama wa Mkoa wa Kilimanjaro 1983-1988, Balozi wa Tanzania katika Nigeria kati ya 1989 hadi 1998 na Balozi wa Tanzania katika DRC kati ya 1998 na 2002 alipostaafu utumishi wa umma.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.


"

MUSUGURI+%2528KULIA%2529+NA+SILAS+MAYUNG President of the United Republic of Tanzania, Mr. Jakaya Mrisho Kikwete has sent a greeting, condolence General of Defence Forces in the country, General Davis Mwamunyange, mourning the death of Lieutenant General (Verse) Silas Peter Dough happened before dawn at 10:30 greet today at the Hospital of Apollo, in New Delhi, India. General dough has died at the age of 71 years.

"I have received with shock and sadness about the death of General Silas dough. Personal Nilimfahamu Manyuga General in his life. He was a brave soldier of our army. He was commander of the reliable defense of our country, "said President Kikwete and add:
"In all your life General Dough demonstrated by proving his patriotism for his country and his dedication to peacekeeping, security and nationality of our country and our nation. Our Army and a key limendokewa pay advice when his advice was still valid.

He added Mr. President: "Even when in the service of the army, General Dough continued to display characteristics similar to patriotism and courage to serve his country in another chance as secretary of the Association of the Province, as the Ambassador of Tanzania in the countries of Nigeria and the Republic of Democratic of Congo (DRC) and even after retirement public service. Our country imempoteza strong public servant and patriot. "

President Kikwete said: "You using Mwanyunge General Davis, Chief of Defence Forces, sincere greetings of condolence following the death of my heart. Through you, please submit multiple greetings and my condolences to the families and relatives of the deceased to the morbidity and father, parent, guardian, and loved them. In addition, through you I would submit my condolences to all soldiers of Tanzania for loss and fellow soldiers and their commander. "

He stressed Mr. President, "Tell the children-the family of the deceased soldiers and all of Tanzania that my heart is with them in this tragedy. Their sorrow is my sorrow. Pray for Allah, Most Gracious, and give heart to patience in this difficult period of mourning. All is His will and can be placed in Paradise Eternal Spirit of the deceased. Ameni. "

Lieutenant General Peter Dough Silas was born Maswa, MC, 1940. He joined the Army of the Tanganyika Rifles January 10, 1963, after completing secondary education in Bwiru Secondary School, Mwanza. Alihitimu course of military officers July 26, 1963, in Israel, and graduated course Unadhimu and commander of the Army in 1973 in Canada and graduate courses of the highest military commander in 1974 in the country.

He was promoted to Lieutenant General June 21, 1995 and before retiring army, December 31, 1995, he became Director of Training at Headquarters of the Army, Director of the Branch of Training Headquarters of the Army, Commander of Brigedi 202 of Tabora, and Commander of the Division of 20 and 30 of the Tanzania Defense Forces (TPDF).

General Manyuga participated actively Battle Iddi Amin in Operation spend where he was commander of the 206th Brigedi and thereafter that the Special Task Force Commander TPDF in Uganda between 1979 and 1980.

Apart from the army, General Public Dough served as Chief of Singida Region in 1977 - 1978, Secretary of the Association of Kilimanjaro Region 1983-1988, Ambassador of Tanzania in Nigeria between 1989 to 1998 and Ambassador to Tanzania in the DRC between 1998 and 2002 was the civil service retirement.


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
December 4, 2011
(image) ...
Google Translate
August 8, 2011
(image) ...
This translation refers to an older version of the source text.