Log in
HakiElimu

HakiElimu

Dar Es Salaam , Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Uwekezaji katika elimu ya awali hauepukiki.Serikali ichukue hatua

DSC04496.JPG
Wanafunzi wa darasa la awali katika shule ya msingi misunkumilo wilayani nkasi wakirudi nyumbani baada ya masomo.

DSC04497.JPG




Elimu ya awali ni muhimu sana hasa kwasababu ni msingi mzuri katika kumtayarisha mtoto kuanza kukabiliana na changamoto za elimu hasa elimu ya msingi kwani humtayarisha mtoto ili kuanza kupenda elimu na hivyo kufanya vyema katika ngazi zinazofuata za elimu kuanzia msingi, sekondari na elimu ya juu.

Kuona umuhimu wa elimu ya awali, Tanzania ilianzisha mfumo wa elimu unaotaka kila shule ya msingi kuwa na darasa la awali ili kuandaa watoto wa watakaoingia darasa la kwanza.watoto hawa huandikishwa elimu ya awali wafikapo miaka mitano au sita ili wafikapo miaka saba wanaaza darasa la kwanza.

WANAFUNZI+WA+MADASA+YA+AWALI+SHULE+YA+MS
Uwekezaji kama huu ni wa kukatisha tamaa katika elimu.Darasa la awali katika shule ya msingi Selous wilayani Namtumbo

Hii ni hatua muhimu sana na kama uwekezaji wa kutosha utafanyika, basi tanzania siku moja itashuhudia ukuaji mkubwa wa kiwangio cha elimu. baadhi ya nchi za Afrika zinazofanya vyema sana katika elimu ya awali ikianzia miaka mitano ya toka mtoto anazaliwa (Early Childhood Education) ni Nigeria,Afrika ya kusini na Ghana ambazo zimewekeza vilivyo katika elimu ya awali (watoto) na matokeo yake yamezifanya nchi hizi kuwa na viwango vya juu vya elimu Afrika nzima.

Ripoti ya mwaka huu (2012) ya Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (Unicef) kuhusu hali ya watoto, inaonesha dhahiri umuhimu wa elimu ya awali katika kupunguza watoto wa mitaani.zaidi ya watoto milioni 200 kutoka nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hushindwa kutumia fulsa za elimu ipasavyo kutokana na mifumo mibovu ya elimu ya awali. 
 WANAFUNZI+WA+MADARASA+YA+AWALI+SHULE+YA+

Hivyo, uwekezaji wa kweli unaozingatia upatikanaji wa huduma muhimu kwa watoto wote ili kutoa fursa sawa ya kujiendeleza na kuweka misingi ya watoto kupenda kusoma ni muhimu sana ili kuinusuru elimu ya Tanzania.

Hivi karibuni ililipotiwa na vyombo vya habari kuwa zaidi ya wanafunzi 5,000 waliofauru na kujiunga na kidato cha kwanza walibainika kutokujua kusoma na kuandika hali inayolalamikiwa kuwa chanzo chake ni uwekezaji mdogo katika shule za msingi inayoanzia na elimu ya awali.






« Previous Next »

Comments (1)

SELESTINE INNOCENT (UDOM-COED) said:
Nikweli elimu ya awali razima iweze kutambuliwa na serikali na wadau wengine wa elimu maana ni msingi mzuri wa maisha ya mtoto,kwani tafiti nyingi zinaonesha kuwa watoto ambao wamepitia elimu ya awali ni wamepata mafanikio zaidi si kwa mambo ya darasani hata katika masuala ya kijamii kwa ujumla, wameonekana kuwa mstari wa mbele hivyo ni wajibu wetu sisi kama wadau wa elimu, wazazi. na serikali kulipa jambo hili umhimu wapekee kwani ni haki ya msingi kwa maendeleo ya mtoto'' MTOTO NI MWALIMU TUMUANDALIE MAZINGIRA ILI AWEZA KUJIFUNDISHA KILE ANACHOKIPENDA'' by Selestine Innocent
December 30, 2012

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.