Envaya

Envaya

Dar es Salaam Flooding Community Survey

Respondent: Promotion of Education Link Organisation (PELO)
Time Submitted: January 29, 2012 at 11:23 PM EAT
Msimbazi bondeni
Inahitajika nguvu ya pamoja kushinikiza serikali kumwondo Yule mfanyabiashara aliyezungusha ukuta eneo la Kigogo sambusa ili mvua za wakati mwingine,maji yake yasizuiliwe na ukuta yakarudia kuingia kwenye nyumba za watu na kusababisha mafuriko.
Naishi maisha ya shida na msamaria mwema mmoja.Amejitolea kunihifadhi katika kipindi hiki kigumu.Mke wangu anakaa kwa mama mmoja ambaye tunasali wote kanisa moja,wakati watoto nao wanaishi kwa ndugu.Ni kama familia imesambaratika.Inaniumiza sana.
Mafuriko yamenisababishia shinikizo la damu.Naanza maisha upya.Nitakosaje kufikiria?
Kuna baadhi ya nyumba nimeona toka mafuriko yatokee mabomba yake hayatoi maji,wakati kabla ya mafuriko zilikuwa zikitoa maji na tulikuwa tukienda kuchota hapo.
Before flooding: dakika 45 hiviNow: saa 1.30
(No Response)
« Previous responseNext response »

« Back to report