Envaya

Envaya

Dar es Salaam Flooding Community Survey

Respondent: Promotion of Education Link Organisation (PELO)
Time Submitted: 29 Mutarama, 2012 at 22:42 EAT
Mtaa: mabibo relini
Tulikuwa na kivuko cha kuvukia kwenda reline kupanda mabasi ambacho kimesombwa na mafuriko.Kipo kivuko kidogo tu cha muda ambacho hata mvua ya kawaida itakaponyesha kitamezwa.Bado hata bila masika kwa udongo kilionao asubuhi tunapanga foleni kupita katika kivuko hiki kwa udogo kilionao.Serikali itusaidie kutengeneza kivuko kama kilichosombwa na mafuriko.
Kama unavyoona narudia kujenga upya karibu nusu ya nyumba yangu iliyobomolewa na mafuriko
Mmomonyoko huu wa udongo ambao umepanua kingo za mto huu ni tishio kwa makazi yetu.Wadau wa mazingira waangalie namna ya kutusaidia kukabiliana na mmomonyoko huu.
Wake zetu walipata shida ya kutafuta maji ya bomba nyakati za mafuriko.Kidogo naona kuna unafuu kwa wakati huu.Hiki nadhani ni kiashiria kwamba vyanzo vya maji viliathiriwa na mafuriko.Yawezekana serikali imechukua hatua.Ila bila hata mafuriko,mabibo maji ya bomba ni tatizo.
Before flooding: Dakika 40 Now: Dakika 40
Sehemu ya nyumba katika mtaa wa mabibo relini iliyoathiriwa na mafuriko ambayo ilibomolewa na mafuriko huku makazi yakiendelea kukabiliwa na changamoto ya mmomonyoko wa udongo katika kingo za mto
Haya ni masalia ya daraja lililokuwa likitegemewa sana na wakati wa mabibo relini wanapokwenda kupanda mabasi ya kwenda tabata,ubungo na buguruni.Kwa sasa kuna daraja la muda ambalo wakati wa masika halitaweza kuwasaidia.Angalia picha zinazofuata utaona daraja la muda lilivyo.
Hili ndilo daraja la muda linalotumiwa na wakati wa mabibo relini.Wakati wa asubuhi ni foleni kwa kuwa watu wawili hawawezi kupishana,inabidi kusubiliana.Angalia picha inayofuata.
Angalia hali ya daraja la muda wanalotumia wakazi wa mabibo relini.Picha inaonyesha mtu akivuka.Hata mvua kidogo tu ikinyesha daraja hili linamezwa.
« Previous responseNext response »

« Back to report