Respondent: | Tanzania Women of Action(Tawa) |
---|---|
Time Submitted: | 1 Februari, 2012 12:47 EAT |
Magulumbasi A
Tejengewe mitaro kwa mpangilio itakayoruhusu maji kutiririka kwa urahisi wakati mvua zikinyesha ,tupewe madawa ya kufanyia usafi mazingira ambayo bado maji hayajakauka na kuhifadhi wadudu,
Mali zote za ndani zilipotea kasoro nguo tu,Tv.radio, kabati 2 , magodoro,vitanda ,vyombo vya jikoni, vyombo vyote vya mamalishe{ biashara ya chakula}sare na vifaa vyote vya watoto wa shule
yamesababisha nikose ajira , sehemu salama ya kulala,magonjwa kwa watoto wadogo waliokuwa wanachezea maji machafu,kukosa choo ,kukosa uelekeo wa maisha na watoto wangu kuathirika kimasomo,kwani wamechelewa kuanza shule kwa kukosa vifaa muhimu vya shule.
maji yetu ni ya visima kutokana na kubomoka kwa vyoo na wananchi wengine kutapisha vyoo vyao wakati wa mafuriko kumesababisha maji yasiwe salama.
Kabla ya mafuriko: dakika 20 | Sasa: sina kazi |
(Hakuna jibu)
« Rudi nyuma kwenye ripoti