WAKIHABIMA imefanikisha ulipwaji wa mishahara ya vibarua 19 waliokuwa wamefanya kazi
na kushindwa kupata mishahara yao kwa wakati tangu May-Juni 2015. wafanyakazi hao walikuwa wamefanya kazi ya kusafisha uwanja wa ndege Masasi na kuahidiwa kulipwa bila mafanikio.
kwa mujibu wa wasaidizi wa kisheria, Donald Simonje na Mwinda Mkwamba waliosimamia mchakato wa ufuatiliaji wa haki hizo kisheria, wafanyakazi hao walikuwa mara zote wakiahidiwa
bila mafanikio wa ahadi zilizokuwa hazina mwisho. Naye kiongozi wa vibarua hao Bw. Yusufu Madonji walikuwa wana hali ngumu sana kimaisha kwani wengi walikuwa na madeni makubwa. Aidha alitoa shukrani kwa niaba ya wenzake na kuwaalika watu wengine wenye shida mbalimbali za kisheria kuja kwenye ofisi ya WAKIHABIMA ili kupata usaidizi.